VIFUNGASHIO VYA BIDHAA BADO NI TATIZO KWA WAJASIRIAMALI WILAYANI GEITA

Share it:
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa uhuru ,Amour Hamad Amour pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Geita ,Mwl Herman Kapufi wakikagua mtambo wa kuchakata Alizeti.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa uhuru ,Amour Hamad Amour akiweka Mbigu za Alizeti kwenye mashine ya kuchakata.

Ubao unaonesha kikundi kilipo.

Wnanchi wakifuatilia zoezi la uwekaji wa jiwe la msingi kwenye kiwanda kidogo cha kuchakata alizeti.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa uhuru ,Amour Hamad Amour akiweka Jiwe la Msingi kwenye Kiwanda kigodo cha kuchakata alizeti



Vikundi vya wajasiriamali Wadogo wadogo bado vinakabiliwa na changamoto mbali mbali likiwemo swala la kukosekana kwa vifungashio vya bidhaa ambazo wamekuwa wakizitengeneza kwaajili ya kuingiza Sokoni Hali ambayo inapelekea kushuka kwa thamani Bidhaa ambazo wanaingiza Sokoni.

Hayo yametokea wakati wa  uzinduzi wa mradi wa kukamua na kusindika mafuta ya alizeti cha Chemamba wilayani Geita ambapo wanakikundi cha ujasiriamali wamekuwa wakikusanya chupa ambazo zimekwisha kutumika na kuwekea mafuta na pia rebo wamekuwa wakitumia kwa kuandika kwa Mkono na sio zile ambazo zinakuwa zinatambulisha shughuli za kikundi pamoja na namba za simu za wahusika.

Kutokana na hali ambayo wamekutwa nayo wanakikundi hao na Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru Amour  Hamad Amour imemlazimu kuagiza Halmashauri husika kukikopesha kikundi hicho fedha ambazo zitawasaidia katika kuboresha shughuli ambazo wanazifanya.

 Akisoma risala na  taarifa  ya Mradi Huo kwa Kiongozi wa mbio za  mwenge uhuru  Afisa kilimo wa halmashauri ya wilaya ya Geita  Jeremia Kengere  amesema uwepo wa mradi huo umehamasisha wananchi kujikita kulima zao hilo la alizeti kwani wengi wao wamenufaika kutokana na kilimo hicho.

 Mkuu wa Wilaya hiyo,Mwl Herman Kapufi ameitaka halmashauri husika kuhakikisha wanakipa kipa umbele kikundi hicho kwa kukiwezesha Mkopo ambao utawasaidia kujikwamua Hali ambayo wanayo kwasasa.
  
Mwenge wa uhuru umezindua na  kutembelea na kuweka jiwe la msingi miradi Kumi Na Moja na kukibizwa wilaya ya Nyangh'wale.

IMEANDALIWA NA MADUKA ONLINE




Share it:

BIASHARA

Post A Comment: