KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE KITAIFA ATOA SIKU MBILI KWA MKANDARASI KUFANYA MAREKEBISHO SOKO LA MAZAO WILAYANI BUKOMBE

Share it:
Wakimbiza mwenge Kitaifa wakikagua Soko la Namonge.

Soko la Mazao la Namonge

Kiongozi wa mbio za mwenge akikagua baadhi ya mabanda kwenye Soko la nafaka la Namonge.

Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Josephat Maganga akionesha  eneo la ukuta wa Ghara kwa Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru.


Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Amour Hamad Amour akitoa maelekezo kwa Mhandisi wa ujenzi wa halmashauri ya Bukombe Chacha Moseti.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge Amour Hamad Amour Akizindua  Soko la Mazao baada ya kuwa ametoa maelekezo ya ukarabati wa soko hilo.

PICHA NA JOEL MADUKA(MADUKA ONLINE)



Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa Amour  Hamad  Amour  amesikitishwa na Ujenzi wa mradi  wa soko la Mazao Namonge   lililopo  wilayani Bukombe  Mkoani Geita  kwa kujengwa chini ya kiwango na hali ambayo imepelekea kuwepo kwa nyufa nyingi kwenye maeneo mengi ya jingo hilo.

Na pia  amemtaka mkandarasi kurekebisha haraka iwezekanavyo kabla ya mwenge wa uhuru kuondoka Mkoani humo huku akimpa siku mbili maeneo yote ambayo yananyufa kufanyiwa ukarabati haraka zaidi.

Kiongozi huyo wa mwenge ameendelea kuwasisitiza   viongozi wa halmashauri kuhakikisha wakandarasi wanakuwepo katika miradi inayozinduliwa,kuwekewa jiwe la msingi na kutembelewa na mwenge wa uhuru ili kujibu changamoto zitokanazo na miradi hiyo.

Mhandisi wa ujenzi wa halmashauri hiyo CHACHA MOSETI  ametoa  taarifa ya mradi huo kwa mwenge na gharama  Sh,581,217,690 hadi kukamilika kwake ambapo Sh,552,156,805.5 ni Fedha za serikali kuu kupitia mpango wa market insfrastructure,value addition and Rural Finance na Sh,29,060.884.5 ni mchango wa Halmashauri.

Aidha mpaka sasa jumla ya fedha zilizotumika ni Sh ,552,156.805.5 ambazo ni fedha za serikali kuu.

Hata hivyo Baada ya kukagua maeneo mbalimbali ya soko hilo  na kujionea ujenzi huo Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa AMOUR HAMAD AMOUR akatoa maagizo.

“Baada ya kukagua mradi huu tumeona mapungufu mengi mradi umepasuka kwenye kuta sasa kwa vile mradi huu umekusudiwa kuwekewa jiwe la msingi na tumemuuliza mkanadarsi hayupo eneo husika wakandarasi wanatakiwa kuwepo kwenye mradi ili kujibu maswali ambayo yatakuwa yakiulizwa Tunamuomba mkandarasi kabla ya risala ya utii kwa 
Mheshimiwa Rais awe amefika uwanjano na tunatoa siku mbili awe amekamilisha ukarabati wa kasoro ambazo tumezikuta “Alisisitiza Hamad.

Wafanyabiashara wa zao hilo Mlalu Bundala na Emmanuel Mhuli Kasuku wamezungumzia umuhimu wa soko hilo litakapokamilika  kuwa litawasaidia kwa kiasi kikubwa ikiwa ni pamoja na kuongeza thamani ya zao ambalo wanalilima.

Kauli mbiu ya mwenge huu ni "Shiriki kukuza uchumi wa viwanda kwa maendeleo ya nchi yetu."

IMEANDALIWA NA MADUKA ONLINE.
Share it:

habari

Post A Comment: