GEITA:POLISI WAONDOLEWA KWA KOSA LA KUCHELEWA KWENYE TUKIO.

Share it:
:
Mkuu wa wilaya ya Geita,Mwl Herman  Kapufi akitoa maelezo  juu ya uhamuzi wa kuhamishwa kwa Polisi waliokuwa wakifanya kazi kwenye kituo cha nyarugusu pamoja na mkuu wa kituo hicho.

Mkuu wa wilaya Mwalimu Kapufi akiomba  baraza la madiwani limpe ushirikiano katika kutekeleza uwajibikaji kwa wananchi.

 
Madiwani wakimsikiliza kwa makini Mkuu wa wilaya alipokuwa akiwaomba kushirikiana nae.

Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Geita,Elisha Lupuga akihaidi kuendelea kushirkiana na Mkuu wa wilaya .



Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi wilaya ya Geita,Barnabas Mapande akielezea juu ya madiwani kushiriki katika swala la ulinzi na usalama kwenye maeneo yao.

Wawakilishi wa vyama vya siasa wilayani Geita ,wakisiliza kile ambacho kilikuwa kikiwakilishwa.



GEITA :Serikali wilayani Geita imewaondoa  askari polisi wa kituo cha polisi Nyarugusu akiwemo mkuu wa Kituo hicho, kwa kile  kinachodaiwa kushindwa kuwajibika katika tukio la ujambazi lilotokea Oktoba 14 mwaka huu baada ya mfanyabiashara wa dhahabu kuvamiwa nyumbani kwake.

Akizungumza katika kikao cha kuwasilisha taarifa za kata kwenye  baraza la madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Geita Mkuu  wa wilaya ya Geita,Mwl Herman Kapufi  amesema askari hao walishindwa kufika eneo la tukio kuwasaidia wananchi ikiwa ni mita chache kutoka kituo cha polisi hali ambayo ilisababisha kutokea kwa ujambazi.

“Wamevamiwa saa sita ya usiku hatua mia 200 kutoka kituo cha polisi wamepigiwa polisi simu zinaita na walichelewa kufika katika tukio hali hii ilionekana ni makusudi nilifika na kamanda wa polisi wa wilaya nimeagiza wale polisi wote waondolewe mara moja na mkuu wao wa kituo”Alisisitiza Kapufi

Diwani wa kata ya Nyarugusu,Swalehe Juma ameelezea kuwa kutokana na jeshi la polisi kushindwa kuwahi katika tukio hilo wananchi walimwomba mkuu wa Wilaya kuwaondoa askari waliopo kituoni hapo kwani wameonekana kushindwa kuwa waangalizi wa mali na usalama wa raia.


Hivi karibuni watu saba (7) wanaodhaniwa kuwa ni majambazi wakiwa na nondo, marungu na mapanga walivamia nyumbani kwa mfanyabiashara wa dhahabu Majaba Masanja mkazi wa Nyarugusu wilayani Geita  na kuchukua dhahabu gramu 860 na kiasi cha fedha zaidi ya shilingi milioni sabini (70).

Imeandaliwa na Madukaonline na Adelina Ukugani.
Share it:

JOEL MADUKA

habari

Post A Comment:

Also Read

ASKOFU WA AIC NCHI AHAIDI KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KWENYE NYANJA ZA KIJAMII

JOEL MADUKA