MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA MJI WA GEITA AUNDA TUME YA UCHUNGUZI YA MWENENDO WA SHULE YA SEKONDARI KASAMWA

Share it:

Mwalimu Mkuu wa shule ya sekondari Kasamwa,Denis Otieno akielezea juu ya tuhuma zilizoandikwa kwenye mitandao  na baadhi ya vyombo vya habari kuwa ameshushwa cheo cha ukuu wa shule akiwa katika ofisi yake shuleni hapo.

Baadhi ya madarasa ya Shule ya sekondari Kasamwa .

Wanafunzi wa shule ya sekondari kasamwa wakitoka madarasani.

Mkurugenzi wa halmashauri wa mji Mwandisi Modest Aporinali akielezea juu ya taarifa za kusimamishwa kwa mwalimu mkuu shule ya sekondari kasamwa.



GEITA:Siku chache kufuatia kusambaa kwa taarifa  katika mitandao mbalimbali ya kijamii na vyombo vya habari kuripoti kuhusu kuvuliwa madaraka kwa Mkuu wa shule ya Sekondari Kasamwa,  Madukaonline imefanikiwa  kufika  shuleni hapo lengo ni kutaka kujua ukweli juu ya taarifa hizo ambazo zimetokana na itikadi ya vyama vya kisiasa.


Madukaonline imezungumza na Mkuu wa shule hiyo, Mwl Denis Otieno ,ameelezea kuwa chanzo cha kuvuliwa madaraka yake na mwenyekiti wa chama cha mapinduzi (ccm)  Mkoa wa Geita Joseph Kasheku maarufu kwa jina la Msukuma ambaye pia ni mbunge wa Geita vijijini ni kutokana na msimamo wake kupiga marufuku kikundi cha wananfunzi cha Magufuli Clabu kufanya sherehe za kuagana(mahafali) shuleni hapo hali ambayo ilipelekea Msukuma kumwagiza   mkurugenzi  wa halmashauri ya mji kumshusha madaraka au kumwamisha kabisa katika Mkoa ambao yeye ni mwenyekiti.


Mwalimu Audax Paul anadaiwa kuwa mlezi wa Magufuli Klabu shuleni hapo alikana kwamba yeye sio hajihusishi na maswala ya chama.

“Mimi ninachofahamu wanafunzi walichangia fedha kwa ajili ya sherehe ya hapa shuleni na lengo lilikuwa sio kufanya sherehe ya Magufuli Klabu ninachojua vijana wengi wa hapa kasamwa wapo kwenye hii Klabu ya Magufuli na lengo lilikuwa ni kumuunga mkono Rais Magufuli ili apite kwenye uchaguzi hayo mambo mengine mimi siyafahamu”alielezea Audax

Hata hivyo madukaoline  imebaini kugawanywa kwa wanafunzi wa kidato cha nne ambao wanatarajiwa kuanza  kufanya mitihani ya  taifa mwezi wa kumi na moja (11) tarehe moja(1) mwaka huu, ambapo baadhi yao wapo kwenye Magufuli Klabu na wengine hawapo.

Willson Lugema ni mwanafunzi wa kidato cha nne shuleni hapo amesema kuwa kulikuwa na vitisho kutoka kwa mwalimu ambae ni mlenzi wa Klabu hiyo kuwa kama wasingechangia wangelifelishwa na kwamba wale ambao waliunga mkono harakati hizo wao wangeweza kufaulu hali ambayo ilipelekea kuingia kwa wasi wasi mkubwa kutokana na maneno ambayo walikuwa wakiambiwa na wanafunzi ambao walikuwa wapo klabu hiyo.

Mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa Geita, Mwandisi Modest Apolinary, ameelezea kuwa hadi sasa bado hawajatoa barua ya kumshusha cheo mwalimu huyo, na kwamba ameunda tume ya kuchunguza mwenendo na nidhamu ya shule hiyo na pindi watakapokuwa wamebaini matatizo yaliyopo ndio watatoa maamuzi ambayo yatakuwa na ushahidi wa juu ya swala la nidhamu shuleni hapo na kwamba mkuu wa shule ni vyema akaendelea na majukumu yake ya kikazi ya kila siku hadi pale watakapokuwa wamemaliza uchunguzi wao.

Shule ya sekondari kasamwa iliyopo halmashauri ya Mji wa Geita iliazishwa mwaka 2004 na sasa  ina jumla ya wanafunzi 996  kuanzia kidato cha kwanza hadi cha nne na kati yao waliojiunga na Magufuli klabu ni zaidi ya wanafunzi 60 ambao walifanya mahafali nje ya shule oktoba 08 mwaka huu.

Imeandaliwa na Madukaonline.

Share it:

JOEL MADUKA

habari

Post A Comment:

Also Read

HABARI KUBWA KWENYE MAGAZETI YA LEO ALHAMISI 10 MAY 2018

JOEL MADUKA