MGWIRA AITUPIA MADAI SERIKALI YA MAGUFULI

Share it:

Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha ACT – Wazalendo Anna Mghwira amedai kuwa harakati za kudai haki za wanawake na usawa wa kijinsia zimerudi nyuma kwa kias kikubwa katika kipindi hiki cha uongozi wa wamu ya tano.

 Amesema hali hiyo  inatokana na kutozingatia baadhi ya madai muhimu ya wanawake.

Mghwira amesema kuwa miaka kumi iliyopita harakati za wanawake zilipiga hatua kubwa kwa kuwa serikali ilitekeleza suala hilo takribani asilimia 30 hususani uwakilishi katika nafasi za uongozi.

Amesema ajenda ya haki za wanawake inakosa nguvu kwa sasa kutokana na kukosa haki ya kikatiba kuhusu haki ya usawa wa kijinsia ambayo ilipendekezwa katika mchakato wa katiba mpya.

Aidha Mghwira asema licha ya kuwepo kwa jitihada kubwa zinazofanywa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli tangu alipoingia madarakani ikiwemo kurudisha nidhamu kwa watumishi wa umma bado harakati za kumkomboa mwanamke dhidi ya mfumo unaokandamiza haki na usawa zimesahaulika.


Share it:

habari

Post A Comment: