NAIBU WAZIRI MPINA:KILA MTU ANAJUKUMU LA KUTUNZA MAZINGIRA

Share it:
Naibu waziri ofisi ya makamu wa Rais muungano na mazingira Mhe,Luhaga Mpina akitoa maelekezo ya utunzaji wa mazingira wakati alipokutana na kamati ya ulinzi na usalama Mkoani Geita.

Naibu waziri ofisi ya makamu wa Rais muungano na mazingira Mhe,Luhaga Mpina ,akiwasili katika ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Geita na hapa anasalimiana na wakuu wa idara wakiwemo kamati ya ulinzi na usalama Mkoani Geita.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Geita,Celestine Gesimba akitoa taarifa ya Mkoa namna ambavyo imekuwa ikitekeleza swala la uhifadhi na utunzaji wa mazingira mbele ya ,Naibu waziri ofisi ya makamu wa Rais muungano na mazingira Mhe,Luhaga Mpina.

Naibu waziri ofisi ya makamu wa Rais muungano na mazingira Mhe,Luhaga Mpina,akisalimiana na mfanyabiashara wa soko kuu la Geita,huku akiulizia bei ya maembe.




Naibu waziri ofisi ya makamu wa Rais muungano na mazingira Mhe,Luhaga Mpina,akiendelea na kuangalia mazao ambayo yanapatikana katika soko Hilo na hapa akiwa ameshilia majani ya mchai chai,akiwa na Mwenyeji wake ambae ni Kaimu Mkuu wa wilaya ya Geita,ambaye ni Mkuu wa wilaya ya Chato Shabaani Ntarambe.






Naibu waziri ofisi ya makamu wa Rais muungano na mazingira Mhe,Luhaga Mpina,akiwa kwenye soko la samaki ambalo linatarajiwa kubomolewa na kuongezewa ukubwa kutokana na kuwepo na ufinyu kwa wafanyabiashara

Naibu waziri ofisi ya makamu wa Rais muungano na mazingira Mhe,Luhaga Mpina,akitelemka kutoka katika chanzo cha maji kinachofadhiliwa na mgodi wa dhahabu wa GGM kilichopo Nyakanga.





GEITA:Kutokana na kuwepo kwa uharibifu wa mazingira ambayo yamekuwa yakisababishwa na shughuli za kibinadamu Serikali imesema kuwa haitamwonea haya mtu yeyote ambae ataonekana kukiuka na kutofuata sheria na taratibu za usafi  wa mazingira zilizowekwa nchini.

Hayo yamesemwa na naibu waziri ofisi ya makamu wa Rais muungano na mazingira Mhe,Luhaga Mpina katika ziara yake ya kikazi ya siku tatu Mkoani Geita.

Mh,Mpina amesema kuwa sheria zimewekwa kwa ajili ya kusimamiwa na kwamba suala la usafi ni jukumu la  kila mtu na kwamba kutokana na magonjwa ya milipuko ambayo yamekuwa yakijitokeza yamekuwa yakilirudisha nyuma Taifa katika swala la maendeleo.

“Kiongozi Mkuu wa nchi ameshatoa maelekezo sheria zimetungwa na Miongozo imeletwa  siku za kufanya usafi zimewekwa lakini watu hawafanyi usafi hili swala la usafi ni vita  ambayo ni lazima tuipiganie kwa nguvu zote kamwe hatutaweza kuwalazia damu wale ambao wanakiuka sheria za mazingira”Alisisitiza Mpina

Hata hivyo  Naibu waziri ametembelea mtaa wa Katoma ambapo wananchi wamemweleza kuwa hali ya eneo hilo sio nzuri  ni  kutokana na kwamba kuna eneo ambalo mgodi umekuwa ukitiririsha maji kuelekea maeneo ya wananchi hali ambayo imekuwa ikisababisha wananchi kuwa na hofu kutokana na kujaa kwa maji eneo hilo huku wakigusia kuwepo kwa vumbi linalotokana na uchimbaji katika mgodi wa dhahabu wa Geita. (GGM)

Kutokana na malalamiko hayo kutoka kwa wananchi Mh,Mpina ametoa miezi mitatu ya kuhakikisha wanakamilisha mazungumzo na kujua ni wapi mfereji utapita ili uweze   kuelekezea maji yatakapopolekwa na kuondoa kero kwa wananchi ambao wamekuwa na malalamiko ya muda mrefu.

Imeandaliwa na Madukaonline.


Share it:

JOEL MADUKA

habari

Post A Comment:

Also Read

WAZIRI JAFO AAGIZA UJENZI WA KITUO CHA AFYA BWANGA UKAMILIKE NDANI YA MWEZI MMOJA

  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI) Selemani Jafo akiwa na viongozi

JOEL MADUKA