GEITA:WALIOVAMIA MAENEO YA HIFADHI YA MISTU WAPEWA SIKU 14 KUPISHA MAENEO HAYO

Share it:

Naibu waziri ofisi ya makamu wa Rais muungano na mazingira Mhe,Luhaga Mpina,Akizungumza na wananchi waliovamia maeneo ya hifadhi ya mistu wa Geita na kutengeneza makazi katika maeneo hayo.

Naibu waziri ofisi ya makamu wa Rais muungano na mazingira Mhe,Luhaga Mpina,akiangalia maeneo ambayo yamefyekwa na wananchi kwa lengo la kutengeneza makazi kwenye msitu wa hifadhi wa Geita.

Mwenyekiti  wa halmashauri ya Mji wa Geita,Leornad Bugomola,akimweleza Naibu waziri namna ambavyo wakala wa mistu nchini (TFS )Kwa kushindwa kuwaondoa wananchi kwa wakati hadi wanafikia hatua ya kufyeka na kuweka makazi kwenye maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya hifadhi.

Wananchi wakimsikiliza ,Naibu waziri ofisi ya makamu wa Rais muungano na mazingira Mhe,Luhaga Mpina wakati alipokuwa akitoa maagizo ya kuondoka katika maeno waliyovamia

Naibu waziri ofisi ya makamu wa Rais muungano na mazingira Mhe,Luhaga Mpina,Akikagua na kuangalia shughuli ambazo zimekuwa zikifanywa kwenye mgodi wa Coronel Simba alipotembelea kwa lengo la kukagua mazingira na kujionea miundo mbinu.

Naibu waziri ofisi ya makamu wa Rais muungano na mazingira Mhe,Luhaga Mpina,akipatiwa maelezo kwenye  sehemu ambayo imekuwa ikiwekwa kwaajili ya maji machafu yanayotumika kuchenjulia dhahabu


Naibu waziri ofisi ya makamu wa Rais muungano na mazingira Mhe,Luhaga Mpina,akikagua eneo la maji machafu lililopo kwenye mgodi wa Busolwa.

Naibu waziri ofisi ya makamu wa Rais muungano na mazingira Mhe,Luhaga Mpina,akimpongeza Mkurugenzi wa mgodi wa CS,Coronel Simba kwa kuweka mazingiara vizuri kwenye eneo la mgodi wake.





Wananchi wanaoishi kwenye maeneo ya hifadhi ya mistu  Mkoani Geita,wametakiwa kupisha maeneo hayo ndani ya siku kumi na nne (14).

Hayo yamesemwa na naibu waziri ofisi ya makamu wa Rais muungano na mazingira Mhe,Luhaga Mpina wakati wa ziara yake ya kikazi ya siku tatu (3) Mkoani Geita,alipotembelea hifadhi ya pori la mistu ya Geita na kukutana na wananchi ambao walimwomba  Mh,Mpina kuwapatia maeneo ambayo wamevamia na kutengeneza makazi.

Wakizungumza kwa nyakato Tofauti,wananchi hao wamemwomba naibu waziri Mpina kuangalia uwezekano wa kuwaachia maeneo hayo kwani wengi wao hawajapenda kuvamia maeneo ya hifadhi ya taifa ya misitu ni kutokana na ugumu wa maisha ni sababu ambayo imechangia kushindwa kulipia kodi za nyumba kwa wananchi ambao wamevamia hifadhi hizo.

Kutokana na kilio  hicho cha wananchi ikamlazimu Naibu waziri Mpina,Kutoa maelekezo ya wananchi kufuata kanuni na sheria zilizowekwa na bunge pamoja na  nchi ikiwa ni pamoja na kufika katika ngazi zinazohusika pindi wanapohitaji maeneo kwa ajili ya makazi na kuacha dhana ya kuvamia maeneo ya hifadhi bila ya taratibu.

“Sasa kilio  chenu cha kuhusu kwamba mnahitaji kupatiwa sehemu, hilo litakwenda kwa utaratibu mwenyekiti na mkurugenzi wa halmashauri wapo hapa mnaweza kuwaona na wakawasaidi lakini sio kuingia kinyume na kujichukulia maeneo bila ya ridhaa ya serikali kwa hiyo ninawaomba wananchi wangu ondokeni kabla ya hizo siku kumi na nne (14) kumalizika sisi tumewekwa kusimamia sheria endapo tukizivunja nadhani tunaweza kuadhibiwa pia hivyo nawaomba sana mzingatie sheria”alisema Mpina.

Hata hivyo mwenyekiti  wa halmashauri ya Mji wa Geita,Leornad Bugomola,amewashukia wakala wa mistu nchini (TFS )Kwa kushindwa kuwaondoa wananchi kwa wakati hadi wanafikia hatua ya kufyeka na kuweka makazi kwenye maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya hifadhi.

“Hili swala ni lazima tuliweke wazi mimi kama mwenyekiti wa halmashauri ya mji nimeshaagiza mara nyingi na mimi mtu ninayemwagiza ni afisa misitu ninapomwagiza anashindwa kuingia kwenye misitu na kudai kwamba kuna wakala wa misitu wanasema asaiwaingilie kwenye shughuli kwa hiyo hili suala mimi siwezi kumung’unya maneno  wakala wa misitu ana matatizo maana wanawaachia wananchi wanajenga ndio wanakuja kuwatoa baada ya kuwa wameshajenga”alifafanua Bugomola

Naibu waziri mh Mpina amemaliza ziara yake huku akiagiza baraza la mazingira nchini (Nemc) kufanya ukaguzi katika migodi yote midogo lengo likiwa ni kuangalia suala la uhifadhi na utunzanji wa mazingira katika migodi hiyo.

Imeandaliwa na Madukaonline.



Share it:

habari

Post A Comment: