WANANCHI WALIOVAMIA ENEO LA KITUO CHA AFYA KATORO KUVUNJIWA NYUMBA ZAO BAADA YA SIKU SABA

Share it:
Mkuu wa wilaya ya Geita,Mwl Herman Kapufi akitoa maagizo kwa wananchi ambao wamevamia katika eneo la kituo cha afya kupisha ndani ya siku saba kabla ya kuondolewa kwangu

Wananchi wakimsikiliza kwa makini mkuu wa wilaya wakati alipokuwa anatoa maagizo ya kuachia maeneo hayo kwaajili ya ujenzi wa nyumba ya kuhifadhia mahiti

Mkuu wa wilaya ya Geita akikagua maeneo ambayo yamevamiwa na wananchi baada ya kutoa maagizo.

Mganga mfawidhi wa kituo cha afya cha katoro Peter Janga akitoa maelezo kwa mkuu wa wilaya namna ambavyo ujenzi unatakiwa kufanyika kwenye kituo hicho

Mwenyekiti ambaye amemaliza muda wake kwenye mtaa huo,Joel  Mazemule akielezea namna ambavyo wananchi hao walivyoshauliwa kupisha maeneo hayo





Wananchi wa mtaa wa kabahelele Kata ya katoro wamepewa  siku saba kupisha maeneo ambayo wameingia kwenye kituo cha afya hali ambayo imepelekea kuwepo kwa  stofahamu huku wengine wakibubujikwa na machozi ,baada ya mkuu wa wilaya ya Geita,Mwl Herman Kapufi kutoa agizo hilo.

Kaya  ambazo zinatarajia kubomolewa katika zoezi la kupisha eneo hilo ambalo lilivamiwa kinyume na utaratibu ni zaidi ya 28 zenye wakazi  takribani 128

Mkuu huyo wa Wilaya ametoa amri ya wananchi hao kuondoka baada ya serikali kubaini wanaishi ndani ya eneo la Kituo cha Afya Katoro na kwamba zoezi la kubomoa nyumba zao litaanza kutekelezwa Januari 11 siku ya Jumatano ikiwa ni maandalizi ya kujenga uzio na chumba cha kuhifadhia maiti.

Wakizungumza kwa uchungu mbele ya Mkuu wa Wilaya  na katika eneo hilo wakazi wa eneo hilo   Paulina Mtabazi, Stanley Mwigaya, pamoja na Paulo Magala  wamesema wamekuwemo ndani ya eneo hilo kwa muda mrefu, huku wengine wakidai waliuziwa na viongozi wa  vijiji.


Pamoja na maelezo hayo msimamo wa Mkuu wa Wilaya ukawa ni wananchi kupisha maeneo hayo kabla ya jumatano ya wiki ijayo, huku akipinga hoja za   kuongoza muda na kwamba ikifika siku hiyo kikosi cha kutuliza Ghasia FFU kitatia nanga eneo hilo ili kuimalisha ulizi wakati wa zoezi la kubomoa nyumba.


“Mimi sitoi muda leo ninapondoka  wewe tafuta mafundi chukua vitu vyako mbao zako,bati zako na kila kitu nimeongeza siku moja tu jumatano asubuhi FFU na mimi nakuja hapa na siku ya jumanne vifaa vya kubomolea vitakuwepo maeneo haya”alisisitiza Kapufi

Madukaonline  imezungumza na mwenyekiti aliyemaliza muda wake Joel Mazemule ambapo amekili kuwa eneo ambalo wananchi wanalilia ni mali ya serikali na kwamba walishawai kuwaambia wananchi hao kuwa ni vyema wakapisha kwani muda wowote watakuja kutolewa.

“Wakati mimi nikiwa ni mwenyekiti nilishawai kuwaambia kwamba siku yoyote iwe miaka kumi ishirini lazima eneo hilo serikali itakuja kulichukua maana ni mali yake na sio mali yao tatizo ambalo limewaponza wananchi ni kumsikiliza diwani aliyemaliza muda wake Mama Mingisi alikuwa anawaambia wasiwe na wasi wasi matokeo yake ndio hayo ambayo leo yamewakuta”alisema Mazemule

Hata hivyo maamuzi haya yanakuja siku chache baada ya waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na serikali za mitaa (TAMISEMI) George Simbachawene kuagiza eneo la kituo cha Afya lizungushiwe uzio, huku akitaka agizo la Waziri Mkuu kupanuliwa kwa Kituo cha Afya Katoro litekelezwe haraka iwezekanavyo.


Share it:

habari

Post A Comment: