NAPE: WANAHABARI TUMUUNGE MKONO RAIS KATIKA VITA DHIDI YA MADAWA YA KULEVYA

Share it:
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akizungumza na wadau Redio na vyombo vya habari kwa ujumla katika maadhimisho ya Siku ya Redio Duniani yaliyofanyika katika Chuo Kikuu Huria cha Tanzania Jijini Dar es Salaam.


Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye amevishauri vyombo vya habari nchini kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Joseph Pombe Magufuli katika vita dhidi ya madawa ya kulevya nchini.


Ameyasema hayo wakati wa maadhimisho ya Siku ya Redio Duniani yaliofanyika katika Chuo Kikuu huria cha Tanzania na kusisitiza kuwa vyombo vya habari viwe sehemu ya kuwaunganisha watanzania katika mapambano dhidi ya madawa ya kulevya.

“Wanahabari tuliunganishe taifa letu tuwe kitu kimoja katika mapambano dhidi ya madawa ya kulevya” alisisitiza Mhe. Nnauye.

Ameongeza kuwa sasa ni wakati wa watu wote kuungana kwa pamoja zikiwemo tasnia zilizopo katika Wizara yake za Habari Utamaduni Sanaa na Michezo kwani vita hii ni ya watanzania wote na sio mtu mmoja au Serikali pekee.

Aidha Mhe. Nape amevitaka vyombo vya habari kutobaki nyuma katika mapambano dhidi ya madawa ya kulevya na kuhakikisha  haki inatendeka na vita dhodi ya madawa ya kulevya vinashinda.

Imeandaliwa na Na Raymond Mushumbusi WHUSM 

Share it:

JOEL MADUKA

habari

Post A Comment:

Also Read

JUMIA KUWAWEZESHA WATANZANIA KUMILIKI SIMU ZA KISASA KWA BEI NAFUU

Yapunguza bei za simu mpaka 60%! Mteja kuunganishwa na kifurushi cha internet ya bure kutoka Tigo mpaka GB 18 

JOEL MADUKA