RAIS TRUMP ATIA SAHIHI MPYA YA KUZUIA WAHAMIAJI WA KIISLAMU KUINGIA MAREKANI ,HUKU IRAQ IKIONDOLEWA.

Share it:


Rais wa Marekani Donald Trump ametia sahihi amri mpya kuu ya uhamiaji ambayo itawazuia wahamiaji kutoka nchi sita zenye waislamu wengi kuingia Marekani kwa muda wa siku 90.

Iraq imeondolewa kutoka kwa orodha ya nchi saba zilizoorodheshwa awali. Watu wenye visa halali wataruhusiwa kuingia Marekani.

Hatua hiyo ambayo pia inajumuisha marufuku ya siku 120 kwa wakimzi wote, itaaza kutekelezwa tarehe 16 Machi.

Amri ya awali ilifutilia mbali mpango mzima wa uhamiaji wa Marekani, na kuwazuia raia kutoka nchi saba zenye waislamu wengi kuingia Marekani.

Hatua hiyo ilizua fujo kwenye viwanja vya ndege wakati watu wenye stakabadhi halali walizuiwa kuingia Marekani na pia kusababisha maandamano makubwa.

Uongozi wa bwana Trump ulisema kuwa amri hiyo ni muhimu kuwalinda Marekani kutokana na ugaidi.

Ilani ya siku 10 imetolewa ili kusaidia kuzuia fujo zilizoshuhudiwa kwenye viwanja vya ndege tarehe 27 mwezi Januari wakati amri ya kwanza ilipotangazwa.

Wasafiri waliokuwa na visa halali waliokua hewani wakati huo walijipata wakizuiwa na maafisa wa mipaka walipowasili.



Share it:

KIMATAIFA

Post A Comment: