Mkuu wa Wilaya ya Geita Mwl Herman Kapufi pamoja na Sheikh Mkuu wa Geita Alhaji Yusufu Kabaju wakiteta Jambo wakati wa shughuli za baraza. |
Dua ikisomwa wakati wa ufunguzi wa Baraza la kislamu. |
Mwenyekiti wa halmashauri kuu ya BAKWATA Mkoani humo ,Alhaji Said Karidushi ,akielezea tatizo la watumishi kufanyiwa uhakiki kwenye siku kuu ya Idd. |
Ayoub Bwanamadi akisoma Risala mbele ya mgeni Rasmi. |
Kaswida ikiendelea. |
Sheikh Mkuu wa Mkoa huo,Alhaji Yusufu Kabaju akielezea kusikitishwa kwake na taarifa za watumishi kufanya kazi siku kuu ya idd. |
Mkuu wa Wilaya ya Geita Ambaye ndiye alikuwa mgeni Rasmi Mwl Herman Kapufi akielezea juu ya misingi na uhuru wa kuabudu. |
Baraza la
waislamu (BAKWATA) Mkoani Geita limesikitishwa na kitendo ambacho kimeendelea
cha baadhi ya watumishi wa kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Geita kufanyiwa zoezi la kuhakikiwa vitambulisho
vya Taifa na Taarifa za utumishi wa uma kwenye
siku kuu ya idd kitendo ambacho kinaonekana kuingilia uhuru wa kuabudu.
Haya yamesemwa
wakati wa ibada ya baraza ambalo
limefanyika kwenye msikiti wa ijumaa uliopo Kata ya Kalangalala Wilaya na Mkoa
wa Geita Siku ya Jana .
Akizungumza
juu ya hatua hiyo Mwenyekiti wa halmashauri kuu ya BAKWATA Mkoani humo ,Alhaji
Said Karidushi ,amesema kuwa
nchi yetu inaheshimu uhuru wa kuabudu na kwamba swala la wengine kwenda
kuswali na wengine kuakikiwa vyeti ni jambo ambalo sio la kiungwana na wala sio
la kizarendo.
“Nimesikitishwa
sana Mkuu wa Wilaya na Kitendo ambacho leo kimeendelea nimeshahudia kwa macho
yangu watumishi wakifanyiwa uhakiki siku ya leo(jana)Jambo ambalo sio nzuri
nchi yetu imeweka siku ya leo kuwa ya mapumziko kuanzia ngazi mbali mbali za
kiutumishi sasa nasikitika kuona wengine wakiendelea na shughuli swala hili ni
kuwanyima watu haki ya kuabudu”Alisema Karidushi.
Aidha kwa
upande wake Sheikh Mkuu wa Mkoa huo,Alhaji Yusufu Kabaju,amesisitiza kuwa
kitendo ambacho kimefanyika sio kitendo chema na kwamba kwakua kimefika kwa mkuu wa Wilaya
ni vyema wakafanyia kazi ili yasije kujitokeza mambo ya namna hiyo kwa kipindi
cha Mbeleni .
Akijibu
baadhi ya matatizo ambayo yamewakilishwa
mbele yake Mkuu wa Wilaya ambaye ndiye alikuwa mgeni Rasmi kwenye shughuli ya
baraza hilo amesema kuwa mambo ambayo yanashida na ambayo wameyaeleza
hataakikisha anayafanyia kazi kwa kuandika barua ya maelekezo kwa wakuu wa
idara mbali mbali .
Waumini wa
Dini ya Kislamu wamemaliza Mfungo wa siku 30
wa mwezi mtukufu wa ramadhani ambapo ni moja kati ya nguzo muhimu kwenye dini hiyo.
IMEANDALIWA NA MADUKA ONLINE.
Post A Comment: