BAKWATA WASIKITISHWA NA UHAKIKI WA VYETI SIKU KUU YA IDD GEITA.

Share it:
Mkuu wa Wilaya ya Geita Mwl Herman Kapufi pamoja na  Sheikh Mkuu wa Geita Alhaji Yusufu Kabaju wakiteta Jambo wakati wa  shughuli za baraza.



 Dua ikisomwa wakati wa ufunguzi wa Baraza la kislamu.



Mwenyekiti wa   halmashauri kuu ya   BAKWATA Mkoani   humo ,Alhaji Said  Karidushi  ,akielezea tatizo la watumishi kufanyiwa uhakiki kwenye siku kuu ya Idd.

Ayoub Bwanamadi akisoma Risala mbele ya mgeni Rasmi.

Kaswida ikiendelea.

 Sheikh Mkuu wa Mkoa huo,Alhaji  Yusufu Kabaju akielezea kusikitishwa kwake na taarifa za watumishi kufanya kazi siku kuu ya idd.


Mkuu wa Wilaya ya Geita Ambaye ndiye alikuwa mgeni Rasmi Mwl Herman Kapufi akielezea juu ya misingi na uhuru wa kuabudu.

Baraza la waislamu (BAKWATA) Mkoani Geita limesikitishwa na kitendo ambacho kimeendelea cha baadhi ya watumishi   wa  kwenye Halmashauri ya Wilaya ya  Geita kufanyiwa zoezi la kuhakikiwa vitambulisho vya  Taifa na Taarifa za utumishi wa uma kwenye siku kuu ya idd  kitendo  ambacho kinaonekana  kuingilia uhuru wa kuabudu.

Haya yamesemwa wakati wa  ibada ya baraza ambalo limefanyika kwenye msikiti wa ijumaa uliopo Kata ya Kalangalala Wilaya na Mkoa wa Geita  Siku ya Jana .

Akizungumza juu ya hatua  hiyo Mwenyekiti wa   halmashauri kuu ya   BAKWATA Mkoani   humo ,Alhaji Said  Karidushi  ,amesema kuwa  nchi yetu inaheshimu uhuru wa kuabudu na kwamba swala la wengine kwenda kuswali na wengine kuakikiwa vyeti ni jambo ambalo sio la kiungwana na wala sio la kizarendo.

“Nimesikitishwa sana Mkuu wa Wilaya na Kitendo ambacho leo kimeendelea nimeshahudia kwa macho yangu watumishi wakifanyiwa uhakiki siku ya leo(jana)Jambo ambalo sio nzuri nchi yetu imeweka siku ya leo kuwa ya mapumziko kuanzia ngazi mbali mbali za kiutumishi sasa nasikitika kuona wengine wakiendelea na shughuli swala hili ni kuwanyima watu haki ya kuabudu”Alisema Karidushi.

Aidha kwa upande wake Sheikh Mkuu wa Mkoa huo,Alhaji  Yusufu Kabaju,amesisitiza  kuwa  kitendo ambacho kimefanyika sio kitendo chema  na kwamba kwakua kimefika kwa mkuu wa Wilaya ni vyema wakafanyia kazi ili yasije kujitokeza mambo ya namna hiyo kwa kipindi cha Mbeleni .

Akijibu baadhi ya  matatizo ambayo yamewakilishwa mbele yake Mkuu wa Wilaya ambaye ndiye alikuwa mgeni Rasmi kwenye shughuli ya baraza hilo amesema kuwa mambo ambayo yanashida na ambayo wameyaeleza hataakikisha anayafanyia kazi kwa kuandika barua ya maelekezo kwa wakuu wa idara mbali mbali .


Waumini wa Dini ya Kislamu wamemaliza Mfungo wa siku 30  wa mwezi mtukufu wa ramadhani ambapo ni moja kati ya nguzo  muhimu kwenye dini hiyo.

IMEANDALIWA NA MADUKA ONLINE.
Share it:

JOEL MADUKA

habari

Post A Comment:

Also Read

WANANCHI WAJITOLEA KUJENGA SHULE SIMIYU

Wananchi wa Halmashauri ya mji wa Bariadi Mkoani Simiyu wakijitolea kuchimba Msingi wa ujenzi wa vyumba 40 vya madaras

JOEL MADUKA