GGM YATOA VIFAA VYA UJENZI VYENYE THAMANI YA SH MILIONI SABINI(70) KWENYE GEREZA LA GEITA

Share it:
Mkurugenzi wa Mgodi wa dhahabu wa Geita (GGM) Richard  Jordinson Akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Geita Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Kyunga vifaa vya ujenzi.
Mkoa wa Geita Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Kyunga akibadilishana mawazo na Mkurugenzi wa Mgodi wa dhahabu wa Geita (GGM) Richard  Jordinson

Mkuu wa Wilaya ya Geita Mwl ,Herman Kapufi akimkaribisha Mkuu wa Mkoa kwaajili ya ukaguzi wa vifaa ambavyo vimetolewa na GGM.

Mkuu wa Mkoa wa Geita na Mkuu wa Wilaya Hiyo wakikagua vitu ambavyo vimetolewa na Mgodi.






Mkuu wa Magareza Wilayani Geita,Mrakibu Mwandamizi Elly Maiga akishukuru kwa msaada ambao umetolewa.

Mgodi wa dhahabu wa Geita GGM Uliopo Mkoani Geita umefadhili vifaa vya ukarabati wa bomba la maji taka Kwenye Gereza la Wilaya Hiyo vyenya thamani ya Sh Milioni Sabini (70).

Akikabidhi vifaa hivyo Mkurugenzi wa Mgodi huo ,Richard  Jordinson amesema kuwa jumla ya sh milioni sabini zimeweza kugharamia kununua vifaa na kwamba walipokea maombi kutoka kwa Mkuu wa Mkoa na mkuu wa 
Wilaya wakihitaji Mgodi kufadhili vifaa hivyo.

“Tulipokea maombi ya kuombwa kusaidia vifaa vya ujenzi kwenye Gereza la wilaya kutokana na kwamba sisi pia ni jamii na siku sote tunapenda kuona jamii inayotunzunguka inanufaika na uwepo wetu”Alisema Jordinson.

Akipokea vifaa hivyo na kuvikabidhi kwa mkuu wa Gereza Wilaya ya Geita,Mkuu wa Mkoa Meja jenerali mstaafu Ezekiel Kyunga ameushukuru mgodi huo huku akisisitiza ujenzi kufanyika kwa weledi zaidi.

“Tunawashukuru wenzetu wa Geita Gold Mine kwa ushirikiano wao ambao wametuonesha ujenzi ufanyike kwa weledi vile vile thamini ya msaada ambao umetolewa uonekane ili hali ya magereza iwe nzuri pia tuepukane na magonjwa haya ya mlipuko”Alisema Kyunga.

Aidha kwa upande wake Mkuu wa Magareza Wilayani Geita,Mrakibu Mwandamizi Elly Maiga,amesema kuwa baada ya mradi huo kuwa umekamilika utasaidia kuondokana na hali ya magonjwa ya mlipuko kama kipindu pindu na maji taka ambayo yalikuwa yakitoa harufu kali  kwenye Eneo hilo.

Pia  ameendelea kuwaomba wadau wengine kuguswa na kuendelea kuchangia huduma mbali mbali za magerezani kwani changamoto bado ni nyingi.

Gereza la Wilaya ya Geita lilianza mnamo mwaka 1947 wakati huo lilikuwa na uwezo wa kuhifadhi waalifu arobaini na Moja  kadili siku zinavyozidi kwenda linazidi kuwa dogo kwani watu wamekuwa wakifikia idadi ya mia tano hadi mia sita kwa sasa.

IMEANDALIWA NA MADUKA ONLINE


Share it:

habari

Post A Comment: