MWALIMU AFARIKI DUNIA BAADA YA KUTOFAUTIANA KAULI NA MKUU WA SHULE YA SEKONDARI NYIHOGO KAHAMA

Share it:
Walimu wakiandamana
Walimu wakiandamana.
Mwalimu Emmanuel Magema akieleza kwa nini wameandamana
Mwalimu Theresia Mushi akielezea jinsi tukio lilivyotokea
Wanafunzi wakiwa nje ya madarasa baada ya tukio kutokea
Walimu wakielekea kwenye ofisi ya halmashauri ya mji Kahama
Walimu wakiingia katika ofisi za halmashauri ya Mji Kahama
Walimu wakielekea katika ofisi za halmashauri ya Mji Kahama
Picha kwa Hisani ya Kijukuu Blog

Mwalimu wa Shule ya Sekondari Nyihogo iliyopo katika Halmashauri ya Mji wa Kahama mkoa wa Shinyanga Grace Kalinga  (39) amefariki dunia muda mfupi baada ya kudaiwa kujibishana maneno na Mkuu wa shule hiyo Ismail Ally.

Kwa mujibu wa walimu wa shule hiyo, tukio hilo limetokea leo  Ijumaa Oktoba 13,2017 asubuhi majira ya saa tatu baada ya mwalimu Grace kwenda kwa mkuu wa shule hiyo kufuatilia ruhusa ya kwenda masomoni.

Kutokana na tukio hilo walimu hao wameandamana hadi ofisi ya Afisa Elimu Sekondari ili kushinikiza serikali imchukulie hatua za kinidhamu mkuu huyo kutokana na kusababisha kifo hicho ikiwa ni pamoja na kumuundoa katika shule hiyo.

Aidha Walimu hao wamesema mwalimu huyo amekuwa na tabia ya kufanya mapenzi na wanafunzi jambo ambalo linawafedhehesha na kwamba asipoondolewa katika shule hiyo basi wao waondolewe na kupelekwa kwenye shule zingine.

Hata hivyo taarifa zinasema kwamba walimu hao kwa sasa wanaendelea na mazungumzo na katibu tawala wa wilaya ya Kahama Timoth Ndanya katika Ofisi ya mkuu wa wilaya hiyo ili kufikia mwafaka wa suala hilo.

Hata hivyo Mkuu wa shule hiyo Ismail Ally amesema hawezi kulizungumzia hilo kwa sasa kutokana na kuwa katika harakati za Kupeleka taarifa hizo kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji wa Kahama.

Mwili wa Marehemu mwalimu Grace umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika Hospitali ya Mji wa Kahama huku Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo Dokta Fredrick  Malunde akithibitisha kupokea mwili huo.


Share it:

JOEL MADUKA

matukio

Post A Comment:

Also Read

HABARI KUBWA KWENYE MAGAZETI YA LEO JUMATATU 14MAY 2018

JOEL MADUKA