MIKOA YAAGIZWA KUUNDA KAMATI ZA KUSHUGHULIKIA WATU WENYE ULEMAVU

Share it:
Mwenyekiti wa Shirikisho la Vyama vya Walemavu Tanzania(SHIVYAWATA), Bi. Ummy Nderininanga akizungumza na watu wenye ulemavu na wananchi wa Bariadi Mkoani Simiyu (hawapo pichani), wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Watu Wenye Ulemavu Duniani, yaliyofanyika Kitaifa Mkoani humo katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji Bariadi.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Anthony Mtaka akitoa ufafanuzi juu ya masuala mbalimbali kwa Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe.Joseph Kakunda(kulia) na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Walemavu, Mhe.Stella Ikupa(katikati) walipofika Ofisini kwake kabla ya Maadhimisho ya Siku ya Watuwenye Ulemavu Duniani, yaliyofanyika Kitaifa Mkoani humo. 

Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Ndg.Jumanne Sagini akiwasilisha taarifa ya Mkoa kwa Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe.Joseph Kakunda(hayupo pichani) na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Walemavu, Mhe.Stella Ikupa(kulia) walipofika Ofisini kwa Mkuu wa Mkoa huo,kabla ya Maadhimisho ya Siku ya Watuwenye Ulemavu Duniani, yaliyofanyika Kitaifa Mkoani humo. 

Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe.Joseph Kakunda(hayupo pichani) na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Walemavu, Mhe.Stella Ikupa(kushoto)akimjulia hali mmoja wa Wagonjwa waliopata Ajali na kulazwa katika Hospitali Teule ya Mkoa huo, kabla ya Maadhimisho ya Siku ya Watuwenye Ulemavu Duniani yaliyofanyika Kitaifa Mkoani humo. 



Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe.Festo Kiswaga akiwasilisha Salamu za Mkoa kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka, wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Watu Wenye Ulemavu Duniani, yaliyofanyika Kitaifa Mkoani humo katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji Bariadi.

Mmoja wa watu wenye Ulemavu, Bw.Athumani Rubandame aliyepata ulemavu kutokana na ajali za barabarani akitoa ushuhuda juu ya namna ajali za barabarani zinavyochangia ulemavu, wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Watu Wenye Ulemavu Duniani, yaliyofanyika Kitaifa Mkoani humo katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji Bariadi.


Baadhi ya Viongozi na Watu wenye Ulemavu wakimsikiliza Mgeni Rasmi katika Maadhimsho ya Siku ya Watu wenye Ulemavu Duniani, yaliyofanyika Kitaifa Mkoani Simiyu, Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe.Joseph Kakunda(hayupo pichani).

Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Ndg.Jumanne Sagini(katikati) akiteta jambo na Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe.Festo Kiswaga, Mhe.Festo Kiswaga(kulia), katika Maadhimsho ya Siku ya Watu wenye Ulemavu Duniani, yaliyofanyika Kitaifa Mkoani Simiyu, katika Uwanja wa Halmashauri yaMji Bariadi, (kushoto) Katibu wa SHIVYAWATA Ndg.Felician Mkude

Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe.Joseph Kakunda(wa pili kushoto) akicheza pamoja na watu wenye ulemavu  na baadhi ya viongozi , baada ya kumaliza shughuli za Maadhimisho ya Siku ya Watu wenye Ulemavu Duniani, yaliyofanyika Kitaifa Mkoani Simiyu, katika Uwanja wa Halmashauri yaMji Bariadi..



Na Stella Kalinga, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.

Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe.Joseph Kakunda ameiagiza mikoa na Halmashauri zote Nchini kuhakikisha kuwa zinaunda Kamati za kushughulikia mahitaji ya watu wenye Ulemavu katika kila Halmashauri, Kata na Vijiji, kabla ya June 30, 2018.

Mhe. Kakunda ametoa agizo hilo wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Watu wenye Ulemavu Duniani, ambayo yameadhimishwa Kitaifa katika Uwanja wa Halmashauri ya mji Bariadi Mkoani Simiyu.

Amesema Serikali imetenga shilingi milioni 50 kuliwezesha Baraza la wenye Ulemavu Kitaifa kufanya kazi zake kwa mujibu wa Sheria ikiwa ni pamoja na kuhakikisha Kamati zinaundwa hadi ngazi ya vijiji, ili kufanikisha azma hiyo,  amesema lazima ziundwe kamati za kushughulikia wenye ulemavu katika kila Halmashauri, Kata na Vijiji, ambapo ameipongeza mikoa ya Simiyu,, Tabora na Mbeya kwa kukamilisha zoezi hili.

“Naipongeza mikoa ya Simiyu, Tabora na Mbeya kwa kuanzisha kamati hizo katika Halmashauri zao  zote, naagiza Kamati hizo ziundwe katika mikoa yote na katika Halmashauri zote nchini, wale ambao bado hawajakamilisha wakamilishe; tunataka kuona ifikapo tarehe 30 Juni 2018 mikoa yote iwe na kamati hizo” amesisitiza Kakunda.

Mhe.Kakunda pia ameziagiza Halmashauri zote Nchini kuwapa Kipaumbele Wajasiriamali wenye Ulemavu katika utoaji wa Mikopo inayotokana na asilimia 10 ya Mapato ya ndani ili waweze kujipatia mitaji ya kuendeshea shughuli zao mbalimbali za ujasiriamali na kujikwamua kiuchumi.

Ameongeza kuwa Serikali imeandaa utaratibu wa Bima ya Afya kwa watu wote wakiwemo wenye ulemavu ambao ujumuisha upatikanaji wa huduma tengamavu na vifaa saidizi na itaendelea kuagiza na kutoa vifaa hivyo kwa watu wenye ulemavu.

Aidha, amesema Serikali itahakikisha miundombinu inakuwa rafiki na fikivu kwa wenye ulemavu, itaangalia namna bora ya upatikanaji wa ajira kwao,  itawahimiza wamiliki wa vyombo vya habari kutumia wakalimani wa lugha ya alama, kuendelea kuchukua hatua kadi dhidi ya wanaofanya ukatili kwa wenye ualbino, italifanyia kazi suala la ukosefu wa Ofisi kwa ajili ya SHIVYAWATA kwa kuangalia uwezekano wa kushirikisha Halmashauri kutenga Ofisi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa SHIVYAWATA Bi.Ummy Nderininanga akiwasilisha risala ya watu wenye Ulemavu, ametoa mapendekezo kadhaa kwa Serikali na kuomba yafanyiwe kazi ikiwa ni pamoja na watu wenye ulemavu kupatiwa bima za afya,upatikanaji wa ofisi za SHIVYAWATA,  kuongezwa kwa nafasi za ajira kwa watu wenye ulemavu, kutoa mikopo kwa watu wenye ulemavu,kuongeza ulinzi kwa watu wenye ualbino na wanafunzi wa elimu ya juu wenye ulemavu kupewa ruzuku badala ya mikopo, ambayo yote yalitolewa ufafanuzi na Viongozi wa Serikali.

Naye Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anyeshughulikia wenye Ulemavu, Mhe.Stella Ikupa amesema Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali imeanza  kutoa kipaumbele  na kujumuisha watu wenye ulemavu katika mpango wa ukuzaji ujuzi unaoendeshwa na Ofisi ya Waziri Mkuu  na pia imeanza  kujadili kuona ni jinsi gani mikopo ya elimu ya Juu itatolewa kama ruzuku kwa watu wenye ulemavu.

Akiwasilisha salamu za Mkoa kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu  Mkuu wa Wilaya ya Bariadi Mhe.Festo Kiswaga amesema Mkoa wa Simiyu umeweka utaratibu maalum wa kuwatambua watu wenye ulemavu kuanzia ngazi za vijiji na kubainisha kuwa hadi kufikia mwaka 2017 jumla ya watu 6305 wenye ulemavu mbalimbali wametambuliwa.

Maadhimisho ya Siku ya Watu wenye Ulemavu mwaka 2017 yamebeba Kauli Mbiu isemayo , yenye Kauli Mbiu isemayo “BADILIKA TUNAPOELEKEA JAMII ENDELEVU NA IMARA KWA WOTE”  na ni mara ya kwanza kufanyika Mkoani Simiyu.




Share it:

JOEL MADUKA

habari

Post A Comment:

Also Read

HABARI KUBWA KWENYE MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI MACHI 24, 2018.

JOEL MADUKA