KIKUNDI CHA VIJANA WABUNI MRADI WA KUKOPESHANA PIKIPIKI WILAYANI MBONGWE

Share it:
Kiongozi wa mbio za Mwenge wa uhuru Kitaifa Charles Kabeho akimpatia Cheti cha Pongezi  Mwenyekiti wa kikundi cha Upendo Bw, Bilali Mbaraka wakati alipokwenda kuwakabidhi piki piki sita kwenye ofisi zao.
Pikipiki Sita ambazo zimekabidhiwa Kwenye kikundi cha Upendo kilichopo halmashauri ya wilaya ya Mbongwe.

Mbio za mwenge wa uhuru zikiendelea baadhi ya askari wa kikosi cha kutuliza ghasia wakiwa mbele kwaajili ya kuhakikisha ulinzi na usalama wakati wa shughuli ya mbio za mwenge wa uhuru.

Mkuu wa Wilaya ya Mbongwe,Matha Mkupasi akiwapatia Cheti kikundi cha Upendo.

Vijana kumi na mbili(12) kwenye halmashauri ya wilaya ya Mbongwe Mkoani Geita,wamebuni mbinu ya kuchangishana  fedha kwaajili ya kununua pikipiki ambazo wanatarajia  kufanyia shughuli ya ubebaji wa abiria (Boda doda)kwa lengo la kukabiliana na tatizo la ukosefu wa ajira.

Mwenyekiti wa kikundi hicho kinachotambulika kwa jina la  Upendo Bw,Bilali Mbaraka amesema kuwa waliamua kuanzisha utaratibu huo kutokana na kutokupata faida wakati walipokuwa wakikodi au kuajili kwenye shughuli hiyo ya pikipiki na ndipo  walichangishana fedha kwaajili ya kununua piki piki ambazo zitaweza kuwasaidia kujikwamua kimaisha.

Deus Nashon ni moja kati ya vijana ambao wapo kwenye kikundi hicho ameelezea  kwamba kila mwaka  wanamatarajio ya kukusanya kiasi cha shilingi milioni ishirini na nne kwaajili ya kununua pikipiki zingine ambazo zitawasaidia kwa vijana waliobakia kwenye kikundi hicho.

Hata hivyo kwa upande wake afisa maendeleo ya vijana wilayani humo  Ismail Mcharo amewataka vijana ambao awana ajira kubuni mbinu ya kujiunga kwenye vikundi ambavyo vitawasaidia kuomba mikopo na kujiajiri  kwa njia za ujasiria mali.

Akiwakabidhi pikipiki sita  kikundi hicho ,Kiongozi wa mbio za Mwenge Charles Kabeho amewataka vijana hao kufuata  sheria za usalama barabarani ikiwa ni pamoja na  kuvaa kofia ngumu pamoja kuwa waaminifu  kwenye shughuli zao za usafirishaji  wa abiria.

Katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbongwe mwenge wa uhuru umekimbia umbali wa kilmota 160 na kuzindua  pamoja na kuweka mawe ya msingi kwenye miradi 10 ambayo imegharimu kiasi cha sh, bilioni 1.1.


Share it:

JOEL MADUKA

habari

Post A Comment:

Also Read

UNDP YAISAIDIA TANZANIA MFUMO BORA WA KUKUSANYA NA KUHIFADHI TAARIFA ZA HEWA YA UKAWA

Baadhi ya washiriki mafunzo hayo kutoka wizara mbalimbali na vyuo vikuu wakifuatilia mafunzo ya namna ya kutumia

JOEL MADUKA