Bondia maarufu wa ngumi za kulipwa nchini, Thomas Mashali, hatunaye.
Taarifa zinaeleza ameuwawa kwa kupigwa risasi na mwili wake kuokotwa
vichakani maeneo ya Kimara jijini Dar es Salaam, usiku wa kuamkia leo.
Yassin Abdallah maarufu kama Ustaadhi, mmoja wa viongozi wakongwe wa
mchezo wa ngumi amethibitisha na kusema mwili wa Mashali upo kwenye
chumba cha kuhifadhia maiti katika Hospitali ya Rufaa ya Muhimbili
jijini Dar es Salaam.
"Tumethibitishiwa hizo taarifa za majonzi kabisa, mwili upo Muhimbili na msiba upo kwao Tandale," alisema Ustaadhi.
Post A Comment: