GEITA:JAMII NA MASHIRIKA WILAYANI GEITA YAMEOMBWA KUENDELEA KUJITOLEA KUCHANGIA MADAWATI

Share it:
Madawati yaliyotolewa na Shwekelela 


Pankalas Shwekelela akielezea namna ambavyo wameguswa kusapoti madawati katika halmashauri ya mji wa Geita.

Shwekelela na mke wake wakifurahia baada ya kuwa wamekabidhi madawati kwa mkuu wa wilaya ya Geita.


Wanafunzi wa shule ya msingi kalangalala wakifurahia baada ya kupatiwa madawati.

Afisa Elimu Msingi,Catherin Mashala akielezea changamoto ambazo zipo katika wilaya hiyo kwa upande wa elimu.

Mkuu wa wilaya Mwl Herman Kapufi  akitoa maagizo kwa wanafunzi kuakikisha wanaunza madawati hayo ili yaje yawafae kwa baadae.

Mkuu wa wilaya ya Geita,Herman Kapufi akikabidhi madawati kwa mkurugenzi wa halmashauri ya Mji pamoja na baadhi ya wanafunzi.

Wanafunzi Elizabeth John wa shule ya msingi kalangalala akitoa shukrani baada ya kukabidhiwa madawati hayo kwenye shule yao.

Mkuu wa wilaya akimshukuru Bw,Shwekelela na mke wake kwa kuguswa kuchangia maendeleo ya elimu wilayani hapo.
GEITA:Jamii na Mashirika wilayani Geita,yameombwa kuendelea kujitolea kuchangia madawati ili kunusuru wanafunzi kuendelea kukaa chini pindi wanapokuwa masomoni.

Rai hiyo imetolewa na mkuu wa wilaya ya Geita,Herman Kapufi wakati alipokuwa akikabidhiwa madawati 14  yaliyotolewa na familia ya ndugu  Shokelera.

Amesema kuwa  wanafunzi walioandikishwa ni wengi sana kwenye wilaya hiyo  hivyo wengi wamejikuta wakikaa chini na kurundikana madarasani na kushindwa kuelewa kile ambacho wanafundisha pindi wanapokuwa madarasani huku akiwataka wale wote waliotoa ahadi kutekeleza kile walichoahidi.

“Nitoe wito kwa wananchi wa Geita ambao wanajua kwamba tuna watoto wengi sana tuna wanafunzi wengi sana bado tunahitaji madawati waendelee kujitolea”Alisema Kapufi

Aidha kwa upande wake,afisa elimu msingi,Halmashauri ya mji ,Bi Catherin Mashala,ameelezea kuwa madawati hayo kumi na nne (14) ambayo yametolewa yatapelekwa shule ya msingi Kalangalala iliyopo wilayani hapa ili kupunguza msongamano wa wanafunzi kukaa chini.

Kwa upande wake Panklas Shokerela,amesema kuwa wametoa madawati hayo kwa lengo la kuunga mkono jitihada za serikali ya awamu ya tano ya Rais Dk John Magufuli ya kuhakikisha wanaondokana na changamoto ya watoto kuendelea kukaa chini, na kwamba wataendelea kuchangia mambo mbali mbali katika swala la elimu.

Mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa Geita,Mhandisi Modest Apolinary,amewashukuru wadahu ambao wameendelea kujitolea kuchangia madawati katika halmshauri hiyo.


Imeandaliwa na Maduka online blogs.
Share it:

habari

Post A Comment: