GEITA:KAPUFI SINA TATIZO NA MIKESHA YA MAKANISA WALA VIONGOZI WA DINI.

Share it:
Mkuu wa wilaya ya Geita,Mwl Herman Kapufi akizungumza na wachungaji pamoja na maaskofu wa baraza la makanisa ya kipentekoste wilayani Geita,juu ya baraua ya zuhio la mikesha makanisani iliyotoka kwenye ofisi ya mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa Geita.

Akisisitiza juu ya kutokukataza mikesha makanisani kwani anatambua kuwa ni moja wapo ya ibada ambazo zimekuwa zikifanyika kuombea Taifa pia.

Wachungaji na maaskofu wakimwombea mkuu wa wilaya ili Mungu haendelee kumsaidia katika shughuli za kulijenga Taifa pamoja na wilaya ya Geita.

Baadhi ya watumishi wa Mungu wakifatilia kile ambacho kilikuwa kikielezwa na Mkuu wa wilaya ya Geita.

Mwenyekiti wa CPCT ambae pia ni Askofu wa kanisa la FPCT Mkoani Geita,David Nzumbi akimshukuru mkuu wa wilaya kuhuzulia katika kikao chao na kutoa ufafanuazi juu ya katazo la kutokukesha usiku.

Wakiombea Taifa pamoja na Rais John Magufuli katika utekelezaji wa majukumu yake ya kila siku.

Katibu wa CPCT Mkoa wa Geita,Mch Joshua William akimweleza mkuu wa wilaya juu ya adha ambazo wamekuwa wakikutana nazo ikiwa ni pamoja na kurazimishwa kujiunga na jeshi la jadi la Sungusungu.



GEITA:Baraza la Makanisa ya kipentekoste wilaya ya Geita ,limemwomba Mkuu wa wilaya hiyo  kushughulikia katazo la kukesha lililotolewa  mnamo Oktoba 19  lililokuwa likizuia mikesha makanisani kwa vigezo vya Ulinzi na Usalama.

Akinukuu katiba ya nchi ibara ya 19 kipengele cha 1 na 4 ambacho kinatoa haki na uhuru wa kuabudu bila ya kuvunja sheria ya nchi  katika kikao cha baraza hilo na mkuu wa wilaya katibu wa baraza hilo, Mch Joshua Willium ,amesema kuwa  wao pia ni wadawu wa swala zima la amani na wanatambua misingi ya amani katika Taifa.

“Mh,Mkuu wa wilaya tunaamini wewe ni Mwenyekiti wa ulinzi na usalama katika wilaya na pia sisi ni wadau wa amani katika wilaya ,Mkoa na hata Taifa pia tunaomba utusaidie kulishughulikia jambo hili linalotaka kutugawa kwa kutuonyesha kwamba Serikali yetu haipo pamoja nasi,jambo ambalo siyo kweli kwani hata Rais wetu  anatusisitiza tuombe na kumwombea”Alisisitiza Joshua

Kwa Upande wake mchungaji Robert Ngai amesikitishwa na tabia za baadhi ya askari wa jeshi la Sungusungu kwenye Tarafa ya Busanda  kuwalazimisha watumishi wa Mungu ambao ni wachungaji  kujiunga na Jeshi la jadi la Sungusungu huku imani zao zikiwakatalia  kujiingiza katika maswala ya jadi swala hili amemwomba mkuu wa Wilaya kulishughulikia.

Akijibu maombi hayo ambayo ameombwa na baraza hilo kupitia kwa viongozi Mkuu wa wilaya ya Geita,Herman Kapufi amefafanua kuwa yeye hana tatizo na watumishi wa Mungu wala maswala ya mikesha kwani anaamini kuwa ni watu ambao wanaliombea taifa huku akiwataka kutoa taarifa za kupatiwa ulinzi pindi wanapokuwa kwenye mikesha wanapoona kuna viashiria vya uvunjifu wa amani na kuahaidi kushughulikia swala la wachungaji kuombwa kucheza sungusungu.

Imeandaliwa na Madukaonline blogs.



Share it:

habari

Post A Comment: