Mbunge wa viti maalum kwa tiketi ya chama cha demokrasia na maendeleo chadema Upendo Peneza,akiwatunza fedha kwa kuimba vizuri kwaya ya kijiji cha nyakabale |
Mbunge wa viti maalum kwa tiketi ya chama cha demokrasia na maendeleo chadema Upendo Peneza,akiselebuka kwa furuha na wanakwaya ambao walimvutia uwimbaji wao. |
Wananchi waliojitokeza kwenye Mkutano wa hadhara wakimsikiliza mbunge kwa umakini juu ya kile ambacho alikuwa akikizungumza . |
Wananchi wakiunga hoja ya kupatiwa maeneo ya uchimbaji na kuachana na mangwangala ambayo yameonekana kutokuwa na dhahabu. |
Mbunge wa viti maalum kwa tiketi ya chama cha demokrasia na maendeleo chadema Upendo Peneza,akifatilia kwa makini hoja za wananchi zilizokuwa zikitolewa kwenye mkutano huo. |
Mzee ,Kennedy Nyakikelege ,akielezea kusikitishwa kwake na maeneo ambayo yamewekewa bikoni na mgodi wa dhahabu wa GGM. |
Bi,Agnes Peter akielezea masikitiko yake kwa niaba ya wanawake katika kijiji cha nyakabale kutokana na kupangiwa siku za kujifungua. |
Wanawake
katika kijiji cha nyakabale kata ya Mgusu wilaya na Mkoa wa Geita,wamewalalamikia
baadhi ya wahudumu wa zahanati ya kijiji hicho kwa kuwapa siku za kujifungua ambapo siku ya jumamosi na jumapili huduma hiyo
inasitishwa kwa madai kuwa ni siku za mapumziko.
Hayo
wameyasema kwenye mkutano wa hadhara wa mbunge wa viti maalum kwa tiketi ya
chama cha demokrasia na maendeleo chadema Upendo Peneza kijijini hapo,ambapo
wamesemakuwa kumekuwa na kero ya watumishi kupanga siku za mama wajawazito
kujifungua katika zahanati hiyo jambo ambalo linahatarisha maisha ya wajawazito
wengi.
wamesema
kuwa uongozi wa zahanati hiyo ulipanga siku tano za wanawake kujifungua na siku
mbili za jumamosi ni siku za watumishi kupumzika na kuacha maswali kwa wananchi
juu ya wanawake wanaopatwa na uchungu siku hizo kwani hawana sehemu nyingine na
kuwalazimu kusafiri mpaka katika hospitali ya Mkoa
Kutokana
na maelezo ambayo yalitolewa na akinamama hawa ,swala ili limemsikitisha mbunge
wa viti maalum,Upendo Peneza na kuahaidi kufikisha madai yao kwa mkurugenzi wa
halmashari ya mji wa geita kupata ufumbuzi wa jambo hili.
“Nimesikitishwa
sana tabia ambayo wakina mama wamekuwa wakifanyiwa kwa kupangiwa siku ya
kujifungua mimi mama yangu alinizaa siku ya jumamosi ina maana ningepangiwa
siku ya kuzaliwa nisingekuwepo duniani hili swala kamwe hatuwezi kulivumilia
nitahakikisha ninafikisha malalamiko haya kwa ngazi usika”Alifafanua Upendo
Madukaonline imemtafuta mganga mfawidhi wa zahanati hiyo Dkt,
Deogratias Digala, ambapo amekanusha
tuhuma hizo na kusema kuwa muda wowote na siku yoyote huwa wanazalisha
na hayo madai ni kwamba hayana ukweli ndani yake kwani tabia ya kijiji
kuwachongea watumishi kwa viongozi ni jambo ambalo limekuwa nila mara kwa mara.
Sanjali na hayo Mh,Peneza amewaomba wananchi kuungana kwa pamoja
kuomba maeneo ya uchimbaji na kuachana na dhana ya kuendelea kugombea miambataka
maarufu kwa jina la magwangala.
Imeandaliwa na Madukaonline.
Post A Comment: