GEITA:ULAJI MBOVU WA VYAKULA VYA WANGA NI CHANZO CHA UGONJWA KISUKARI

Share it:
Mratibu wa magonjwa yasiyoambukiza Mkoa wa Geita, Dkt Vito Kajoba ,Akizungumza na waandishi wa habari kuhusu swala la lishe ambavyo limekuwa likisababisha magonjwa ya kisukari na presha.

Wananchi waliojitokeza kwenye huduma ya kupima wakisubilia huduma ya kupima afya katika Hosptary ya rufaa ya Geita.



Huduma ya upimaji ikiendelea .
Afisa tawala wa wilaya ya Geita,Saashisha Mafuwe,akiwasisitaza wananchi kujenga desturi ya kupima mara kwa mara na pindi wanaposikia huduma hiyo inatolewa Bure

Dokta Bingwa wa magonjwa ya kisukari Wilayani Geita,Joseph Makuma akielezea hali ilivyo kwa ugonjwa huo Mkoani Geita.




Ulaji wa kupindukia na vyakula vyenye wanga  na mafuta ni sababu ambayo imeelezwa kuchangia kwa kiasi kikubwa magonjwa ya kisukari na presha.

Hayo yameelezwa na mratibu wa magonjwa yasiyoambukiza Mkoa wa Geita, Dkt Vito Kajoba wakati wa zoezi la upimaji wa magonjwa yasiyoambukiza lililofanyika katika hosptali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita.

Amesema kuwa kutokana na dhana ambayo imejengeka kwa wananchi wengi kula vyakula vyenye mafuta mengi na kutokuwa na mpangilio wa ulaji ni sababu moja wapo ambayo imekuwa ikisababisha kuwepo kwa magonjwa  ya kisukari na presha, na hivyo ameshauri ili kuepukana na magonjwa  hayo ni vyema kwa jamii kujenga desturi ya kufanya mazoezi mara kwa mara.

“Tuchukue hatua zifuatazo kwanza turekebishe lishe vyakula vyetu vya mafuta na vyenye wanga mwingi tutumie kidogo sana lakini pia tufanye mazoezi ili kupunguza mafuta ambayo yanakuwa yamerundikana mwilini”Alisisitiza Kajoba

Kwa upande wake afisa tawala wa wilaya ya Geita,Saashisha Mafuwe,amewasisitaza wananchi kujenga desturi ya kupima mara kwa mara na pindi wanaposikia huduma hiyo inatolewa Bure ni vyema wakajitokeza kwa wingi kuangalia afya zao.

Hata hivyo kwa upande wao wananchi ambao walikuwa wamejitokeza katika zoezi la upimaji wameishukuru Serikali huku wakiomba huduma hiyo kupelekwa  na maeneo ya vijijini.
Pamoja na zoezi la upimaji  wa magonjwa yasiyoambukiza bado wananchi wanakabiliwa na changamoto ya kutopata dawa na huduma za kiafya pindi wanapokuwa wameathirika.


Share it:

habari

Post A Comment: