GGM YAKABIDHI MADAWATI ELFU MBILI(2000)KWENYE WILAYA YA GEITA

Share it:
q

Mkurugenzi mtendaji wa GGM,Terry Mulpeter akikabidhi madawati kwa mkuu wa wilaya ya Geita,Mwl Herman Kapufi pamoja na wanafunzi wa shule ya msingi mseto iliyopo Mkoani Geita.
Madawati yaliyotolewa kwenye wilaya ya Geita,yakikaguliwa na Meneja mwandamizi wa maswala ya jamii,Manase Ndoroma pamoja na wafanyakazi wa GGM kabla ya kuyakabidhi kwa mkuu wa wilaya.


Afisa elimu msingi halmashauri ya mji wa Geita Bi, Catherin Mashala ,Akielezea uhaba wa madawati katika halmashauri hiyo.

Mkurugenzi Mtendaji wa GGM,Terry Mulpeter akizungumza namna ambavyo mgodi huo utakavyoendelea kutoa sapoti na kuchangia swala la elimu Mkoani Geita.

 Meneja mwandamizi wa maswala ya jamii,Manase Ndoroma,akifafanua juu ya wao kuguswa kutoa madawati 

 

Mkuu wa wilaya ya Geita,Mwl Herman Kapufi  akimpongeza Mkurugenzi Mtendaji wa GGM,= Terry Mulpeter kwa kutoa msaada wa madawati
Mkuu wa wilaya akiwasisitiza wanafunzi pamoja na walimu kutunza madawati yanayotolewa na wahisani na wadau mbali mbali wa elimu wilayani humo.

Wanafunzi wakipata picha ya pamoja na mkuu wa wilaya pamoja na mkurugenzi mtendaji wa GGM





Jumla  ya madawati elfu mbili (2)  yametolewa  katika wilaya ya Geita, na kampuni ya uchimbaji  wa  Madini ya dhahabu ya Geita(GGM) lengo likiwa ni kutatua changamoto za wanafunzi kuendelea kukaa chini na kubanana pindi wanapokuwa darasani.

Akizungumza katika zoezi la kukabidhi  madawati hayo kwa Mkuu wa wilaya ya Geita,Meneja mwandamizi wa maswala ya jamii,Manase Ndoroma, amesema  kuwa wametoa  madawati  hayo kama sehemu ya kuimarisha elimu  kwenye jamii na mahitaji makubwa kwa sasa hivi katika jamii ni swala la kupunguza watoto kukaa chini hali ambayo imekuwa  ikisababisha wanafunzi kushindwa  kufanya  vizuri katika  masomo  yao.

“Tumetoa madawati haya kama sehemu ya mchango wetu wa kuimarisha elimu katika jamii tunajua kwa sasa hivi mahitaji makubwa katika jamii ni kuwepo kwa madawati”Alisema Manase

Aidha kwa upande wake Afisa elimu msingi halmashauri ya mji wa Geita Bi, Catherin Mashala ameelezea kuwa sekta ya elimu  inakabiliwa na changamoto kubwa  ya upungufu wa madawati hivyo kupelekea baadhi ya wanafunzi  kukaa chini, na kuongeza kuwa wilaya ya geita ina jumla ya wanafunzi  laki 2,24,350 na hivyo kwa kanuni za kielimu wanahitaji madawati elfu  80,770  na  madawati yaliyopo ni elfu 47,123 upungufu  ni  elfu  33,839

Wanafunzi  wa  shule ya msingi mseto, Gedion Joseph na Eva Johanes wameishukuru kampuni ya GGM kwa kuweza kujitoka kusaidia swala la elimu na pia wameahaidi   kuendelea kuyatunza  madawati  hayo ili yaje yawasaidie wanafunzi wengine ambao watakuja    kuyatumia.
Mgeni rasmi katika shughuli ya makabidhiano ambae ni mkuu wa wilaya ya Geita,Mwl Herman Kapufi, amewataka wanafunzi  na  walimu kutunza madawati ambayo watu binafisi na makapuni yamekuwa yakijitoa ili yaje  yawe msaada kwa wanafunzi wengine

Kampuni ya dhahabu ya GGM ,imekwisha kusaidia swala la elimu kwa kujenga shule ya kisasa ya Sekondari ya wasichana ya Nyankumbu,maktaba,pamoja na kurekebisha shule zilizoezuliwa na kuchangia  madawati  Mkoani Geita.


Imeandaliwa na Madukaonline

Share it:

habari

Post A Comment: