WANANCHI MKOANI GEITA WAMETAKIWA KUTUMIA FURSA AMBAZO BADO HAZIJAFIKIWA NA WATU WENGINE

Share it:

Mchungaji wa kanisa la Last church of God Mkoani Geita,Ezekiel Mayala akiongoza ibada ya uzinduzi wa Kiwanda kidogo cha kukoboa mpunga cha Kaboja katika sherehe za uzinduzi.

Baadhi ya wageni waalikwa katika shughuli ya uzinduzi wa kiwanda hicho wakifatilia kile ambacho kilikuwa kikiendelea.

Wakurugenzi wa kiwanda hicho,Bw &Bi Emmanuel Kaboja wakiwakaribisha wageni waalikwa kwenye shughuli ya uzinduzi.

Mitambo ya kukoboresha Mpunga na kupembua ikiwa bado hijazinduliwa 


Diwani wa kata ya Buhala hala ,Mussa Kabese ambae alikuwa ndie mgeni rasimi kwenye uzinduzi huo akikata utepe kuhashiria kuwa amekwisha kukizindua kiwanda hicho kufanya kazi.


Mkurugenzi wa Kaboja Rice Mill,Emmanuel Kaboja akikagua mashine hizo pamoja na mgeni rasmi.

Diwani Mussa Kabese akiwasha mashine  ili kujua kama mitambo inafanya kazi kwa ufasaha.

Hapa akiangalia namna inavyokoboa mpunga mashine hiyo.

Baadhi ya wananchi wakiangalia mitambo ya kukoboa mpunga.


Diwani Musa Kabese akisisitiza jamii Mkoani Geita ,kuchangamkia fursa zilizopo Mkoani humo na kuchana na dhana ya kujua dhahabu ndio fursa pekee.

GEITA:Wananchi wilayani na mkoani Geita,wametakiwa kutumia fursa ambazo bado hazijafikiwa na watu wengine ikiwa ni pamoja na kuwekeza katika viwanda vidogo ili kujikwamua katika janga la ukosefu  wa ajira.
Wito huo umetolewa na diwani wa kata ya Buhalahala , Mussa Kabese wakati wa uzinduzi wa kiwanda kidogo cha kukoboa 
mpunga  cha Kaboja  kilichopo eneo la mwatulole.

Amesema kuwa ni vyema kwa wananchi kuwa na mtazamo tofauti na kwamba fursa pekee sio dhahabu tu katika mkoa wa Geita kwani bado kuna mambo mengi ya msingi ambayo yanaweza kuleta faida na kutoa ajira kwa vijana ambao hawana ajira.

“Kumekuwepo na dhana kwa wananchi mkoani Geita hata kwenye kata ninayoiongoza ya Buhalahala kuona kwamba fursa pekee iliyopo Mkoani hapa ni madini ya dhahabu tu kumbe sio kweli kuna fursa nyingi sana leo tumeona mwezetu Kaboja ameweka mashine ya kisasa ya kukobolesha mpunga na naamini ataajiri vijana hivyo atakuwa amesaidia swala la upungufu wa ajira nchini niombe wananchi kuwa na mawazo nje ya box kwa kuziona fursa na kuzitumia kama ilivyo kwa maeneo mengine”alisema Kabese.


Kwa upande wake ,mkurugenzi wa kiwanda hicho Emmanuel Kaboja,ameelezea  kuwa lengo lake la kufungua kiwanda hicho kidogo cha kukoboa mpunga ni kutoa ajira kwa watanzania ikiwa ni pamoja na kuongeza pato la Taifa.

“Mimi ni mfanyabiashara wa mashine kwa muda mrefu nilianzia mashine ya kukoboa na kusaga mahindi na kusambaza unga wa sembe lakini mtaji ulipokuwa nimeona ni vyema nikafungua  mashine hii ya kukoboa mpunga ambayo nina amini itatoa fursa kwa baadhi ya vijana kuajiliwa hapa na kuinua kipato kwa Taifa na familia”alifafanua Kaboja.

Aidha kwa upande wake bi,Rebeca Emmanuel ambae ni mke wa mkurugenzi wa kiwanda hicho ,amewashauri wakina mama kuwa na ushauri mzuri kwa wanaume katika swala la  maendeleo hili kujinasua kutoka katika hali ya utegemezi katika familia zao.

“Natambua Kuwa mwanamke anamchango mkubwa sana kwenye maendeleo ya mwanaume niwaombe wanawake wenzangu wawe tayari kuwashauri wanaume kubuni miradi ambayo italeta faida kwa akina baba na familia kwa ujumla”alisema Rebeca.

Imeandaliwa na madukaonline blogs



Share it:

habari

Post A Comment: