WATU WAWILI WAMEUWAWA KWA NYAKATI TOFAUTI MKOANI GEITA

Share it:
Kamanda wa Polisi Mkoani Geita Mponjoli Mwabulambo akizungumza na waandishi wa habari juu ya  matukio hayo.
Watu wawili wameuwawa kwa nyakati tofauti Mkoani Geita,ambapo tukio la kwanza lilitokea Novemba 6 katika kijiji cha magiri kata ya Kasenga Wilaya ya Chato,tukio linguine limetokea kijiji cha Buyagu kata ya Nyakamwaga,tarafa ya Busanda wilaya ya Geita,ambapo mwanaume alimuua mke wake na kitu cha ncha kali kwa kile kinachoelezwa ni wivu wa mapenzi.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kamanda wa polisi Mkoani Geita,Mponjoli Mwabulambo amewataja waliuoawa ni Lucia Yagalaza(43)Mkazi wa Buyagu, shughuli ni Mkulima na Ndilachuza Kengere(80)mkazi wa kijiji cha magiri, shughuli ni mkulima.

Amesema tukio la kwanza ambalo lilitokea tarehe sita ambalo liliondoa uhai wa Ndilachuza Kengere marehemu akiwa nyumbani kwake sebuleni aliuwawa na watu wasiofahamika  kwa kunyongwa hadi kufa kwa kutumia kamba ya chandarua na kisha kupakwa unga usoni na watu hao kutokomea kusikojulikana.

Jeshi la Polisi linaendelea na msako mkali ili kubaini kiini cha tukio hilo na kuwatafuta wale ambao wameusika na kifo hicho.

Kamanda Mponjoli,ameendela kuelezea kuwa tarehe 8,Lucia Yagalaza(43) aliuawa na mume wake aitwaye Charles Isamwile kwa kukatwa na kitu chenye ncha kali kichwani akiwa amelala kitandani,mara baada ya kufanya mauaji hayo mtuhumiwa alienda kuwaaga watoto wao ambao walikuwa wamelala nyumba nyingine kuwa anasafiri ingawa hakusema anakwenda wapi wala hakuwataarifu kuhusu kuuawa kwa mama yao.

Kamanda ameongezea kuwa uchunguzi wa kina unaonesha kuwa chanzo cha tukio ni ugomvi wa kifamilia uliotokana na marehemu kumtuhumu mtumiwa kuuza shamba lao bila ya kumshirikisha ,katika eneo la tukio kulikuwa na shoka ambalo lilikuwa na damu ambalo linasadikika kutumika katika mauaji hayo.

Mtuhumiwa amekwisha kukamatwa na yupo mahabusu muda wowote atapandishwa kizimbani kujibu mashitaka yanayomkabili.
Kamanda ametoa wito kwa wananchi kuacha tabia ya kujichukulia sheria mkononi na kwamba kama kuna mambo ambayo ni mazito ni bora wakafika kwenye vyombo vya sheria ili kupatiwa msaada wa kisheria.


 Imeandaliwa na Madukaonline Blogs



Share it:

matukio

Post A Comment: