RIDHIWANI ALAANI VITENDO VYA KUPIGANA WAKULIMA NA WAFUGAJI

Share it:


Ndugu Augustino Mtitu mkulima wa kitongoji cha Upangwani, Kijiji cha Dodoma Isanga, Kata Ya Masanze Jimbo la Mikumi aliyechomwa Mkuki na wafugaji wa kwanza kushoto.


Kwanza niruhusu nikupe Pole ndugu yangu kwa lililokukuta. La msingi Serikali inatakiwa kujua, tunaposema maoni yetu pale Bungeni tunamaanisha. yako mambo unaweza yafanyia utani lakini hapa tulipofika si kwa kuchukulia mzahamzaha. 

Waziri muhusika haya hauyaoni au niliposimulia juu ya Wananchi wa Jimbo la Chalinze kupigwa , kuvunjwa migongo na mwengine kupigwa mshale wa goti na kumpa ulemavu wa maisha mlidhani natania. Sasa hili liwe fundisho. Serikali ni lazima ije na majibu sahihi juu ya kunusuru vita ya wenyewe kwa wenyewe .
 
Jana mtu kavunjwa mgongo, mwengine mlemavu leo kapigwa mkuki wa mdomo umetokea shingoni. Lini tutasikia kilio hiki? Serikali sikieni kabla Damu ya watanzania wanyonge wanaotegemea kilimo kama kiinua mgongo chao hawajapotea. Kuna sheria, na mipango ya matumizi bora ya Ardhi. Nini kinafichwa? 
 
Binafsi Nalaani Vitendo hivi na kuiasa Serikali yangu kujipanga vizuri kabla mambo hayajaharibika. yalianza Kilosa, Mvomelo, Chalinze, Handeni,Kiteto na sasa Mikumi ( kutaja maeneo machache) .Serikali jipangeni, kabla hapajachafuka.
 
RIDHIWANI KIKWETE

MBUNGE WA JIMBO LA CHALINZE.
Share it:

JOEL MADUKA

habari

Post A Comment:

Also Read

MIAKA 22 BILA MV BUKOBA

MV Bukoba ilikuwa moja ya meli kubwa katika ziwa Victoria. Ilikuwa ina uwezo wa kusafirisha watu zaidi ya 400 na tani

JOEL MADUKA