Wananchi wa
Dar es Salaam wakiongozwa na Bonifance Jocob (Mstahiki Mayor wa Manispaa ya
Ubungo) wamemshitaki Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaa Daudi Bashite (Paul Makonda)
kwenye Tume ya Maadili ya Viongozi wa
Umma
Makonda
anatuhumiwa kwa makosa matano ambayo ni Kughushi vyeti vya elimu yake,
kujipatia mali kwa udanganyifu,kukiuka maadili ya Viongozi wa Umma, matumizi
mabaya ya madaraka pamoja na kuvamia kituo cha radio Clouds fm.
Akizungumza
na waandishi wa habar njee ya ofisi za Tume hiyo Boniface amesema tayari
amekabidhi malalamiko yao kwenye ofisi
ya Kamishna kwa ajili ya hatua zingine ambazo wao wataona zinafaa.
Boniface amesema " Tayari nimekabidhi malalamiko
yangu ambayo nimeambatanisha na vielelezo vyote ambavyo vitatumika kama ushaidi
wa awali hivyo ninawaacha Tume wafanye kazi yao."
Boniface
amesema kama Tume wakihitaji ushaidi zaidi yupo tayari kuthibitisha ili Mkuu
huyo wa Mkoa awajibishwe kutokana na
tuhuma zinazo mkabiri
Post A Comment: