WAANDISHI WA HABARI WAASWA KUANDIKA HABARI ZA MAENDELEO

Share it:
Waziri wa Habari, Utamaduni, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe akila kiapo mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo Jijini Dar es Salaam. Wapili kushoto ni Katibu Mkuu Kiongozi Mhandisi Balozi John Kijazi.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi hati ya kiapo Waziri Mpya wa Habari, Utamaduni, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe katika hafla iliyofanyika leo Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi akila kiapo mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo Jijini Dar es Salaam. Wapili kushoto ni Katibu Mkuu Kiongozi Mhandisi Balozi John Kijazi.

Balozi Dkt. Abdallah Saleh Possi akila kiapo mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo Jijini Dar es Salaam. Wapili kushoto ni Katibu Mkuu Kiongozi Mhandisi Balozi John Kijazi. Balozi Dkt. Possi ameapishwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na viongozi walioapishwa katika hafla liyofanyika leo Ikulu Jijini Dar es Salaam. Kutoka kushoto ni Kamishna wa Sekretarieti ya Maadili Jaji Mstaafu Harold Reginald Nsekela, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Mhandisi John Kijazi, Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan,Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahim Juma, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mwanasheria Mkuu wa Serikali George Masaju.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewaasa waandishi wa habari nchini kuandika habari zinazohamasisha maendeleo ya nchi badala ya kuandika habari ambazo hazina manufaa kwa taifa.

Akizungumza wakati ya hafla ya kuwaapisha mawaziri, mabalozi pamoja na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Ikulu jijini Dar es Salaam leo, Rais Magufuli alisema kuwa waandishi wa habari wanatakiwa kuwa wazalendo kwa kuandika habari za kuhamasisha wananchi kushiriki katika shughuli za maendeleo pamoja na kuunga mkono jitihada mbalimbali za Serikali.

“Nchi yetu ina sifa nzuri nje, Rais wa Benki ya Dunia alipotembelea katika nchi yetu hivi karibuni alitupatia  jumla ya shilingi trilioni 1.74 na benki hiyo ipo mbioni  kutupatia fedha nyingine shilingi trilioni 2.8, lakini vyombo vyetu vya habari haviandiki kwa mapani juu ya taarifa ” alisema Rais Magufuli.

Alibainisha kuwa fedha hizo zitatumika katika miradi ya Ujenzi wa barabara za juu eneo la Ubungo, maboresho ya miji, pamoja na Vyuo Vikuu vya  Sokoine na Mandela  na kuleta maendeleo ya nchi yetu lakini taarifa zake hazikupewa uzito unaostahiki katika vyombo vya habari.

Rais Magufuli aliwataka wamiliki wa vyombo vya habari pamoja na waandishi wa habari kufuata uweledi wa taaluma ya habari pamoja na kuweka mbele maslahi ya taifa badala ya maslahi ya mtu mmoja mmoja.

Aidha, Rais Magufuli amewapongeza viongozi aliowaapisha  na kuwataka kufanyakazi kwa bidii na juhudi ili kutimiza azma ya serikali ya kuwa nchi ya uchumi wa kati kwa kutekeleza agenda ya viwanda.

Viongozi walioapishwa ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe, Waziri wa Katiba na Sheria Prof.  Palamagamba Kabudi na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Alfayo Kidata.

Wengine ni Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani Dkt. Abdallah Possi, Balozi wa Tanzania nchini Israel Job Masima, Balozi wa Tanzania nchini Comoro,  Sylvester Mabumba pamoja na Kamishna wa Tume ya Utumishi wa Mahakama Stellah Mugasha.

Na. Immaculate Makilika- MAELEZO



Share it:

JOEL MADUKA

habari

Post A Comment:

Also Read

WANANCHI MKOA WA GEITA WATAKIWA KUJITOKEZA KWA WINGI KWENYE KAMPENI YA ELIMU KWA MLIPAKODI

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Mhandisi Robert Luhumbi akizungumza na waandishi wa habari leo mkoani humo kuhusu Kampeni M

JOEL MADUKA