WANANCHI WAJITOLEA KUTENGENEZA BARABARA YA MTAA MJINI GEITA.

Share it:
Wananchi wa mtaa wa Nyantorontoro "A"Kata ya Nyankumbu wakikwa kwenye shughuli ya kujitolea ya utengenezaji wa Barabara.


Shule ya Msingi ambayo wananchi wamejitolea kutengeneza Barabara ya kufika shuleni Hapo.

Mwenyekiti wa Mtaa wa Nyantorontoro Gerevas Kayelelo kulia akifokeana na moja kati ya wananchi ambaye hakutaka eneo lake kuondolewa mihogo ambayo alikuwa amepanda.


                              Elias Totoe mkazi wa nyantorotoro akizungumza namna ambavyo wameweza kufikia uwamuzi wa kutoa maeneo yao kwaajili ya maendeleo ya mitaa.

Lecta Maningu mkazi nyantorotoro akieleza juu ya tatizo la maji ambavyo limekuwa ni changamoto katika kata hiyo.

Wananchi wakionesha vitendea kazi

 Gerevas Kayelelo m/kiti mtaa wa Nyantorotoro A,akifafanua juu ya uwamuzi wa wananchi kujitokeza kwenye shughuli ya utengenezaji wa barabara.





Barabara ni moja  Kati ya huduma  muhimu za kijamii zinazohitajika  ili kuchochea kasi ya maendeleo lakini maeneo yaliyo mengi  hususani kwenye mitaa kumekuwepo na  changamoto ya miundombinu hiyo ambayo inarahisisha kasi ya maaendeleo.

Kutokana na hali hiyo wananchi wa mtaa wa nyantorotoro “A”  kata ya Nyankumbu halmashauri ya mji wa Geita wamejitokeza  kutengeneza barabara ya kiwango cha molamu  yenye kilomita zipatazo mbili kuelekea kwenye taasisi ya shule mpya ya mtaa huo.

Baadhi  ya wananchi wamezungumza na mtandao wa Maduka Online na kwamba wamejitolea kutengeneza  Barabara kwa ushirikiano ni kutokana na muda mrefu kutokuwepo kwa barabara na shule kwenye mtaa huo.

“Kiukweli watoto wetu wamepata shida kwa muda mrefu na kusoma umbali wa kilomita nyingi kutokana na shule kukamilika tumeonelea basi sisi pamoja na mwenyekiti wetu wa mtaa kuweka jitihada za kutengeneza barabara ambayo itaelekea shuleni na itawasaidia watoto wetu kutembea kwa ukaribu kufuata elimu”alisema Lecta Maningu.

 “Pamoja na kwamba sisi kama wananchi tumejitolea kujenga barabara ambayo inaelekea shuleni lakini tunaiomba serikali yetu kupitia kwa Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji kuona umuhimu wa kuweka maji shuleni hapo ili kupunguza adha kwa wanafunzi shuleni hapo kwani hakuna maji”aliomba  Bi, Cesilia Clement

Lakini pamoja na  baadhi ya wananchi kutoa maeneo yao kwa hiyari  ili kupitisha barabara, wapo wengine wanakwamisha juhudi za wengi kufikia malengo hayo, kama mzee aliyetambulika kwa jina la Mayenga  ambaye ameonekana mgumu wa kutoa eneo lake lililolimwa mihogo jambo ambalo limesababisha  malumbano makali baina yake na wananchi.

Mwenyekiti wa Mtaa huo Gerevas Kayelelo, alisema kuwa wananchi wake wametoa ardhi yao kwa ajili ya barabara bila kuomba hata fidia ya aina yoyote.

Pamoja na kutokuwa na muafaka baadhi ya wananchi wamelalamikia kitendo cha Bw Mayenge kuwa ni moja Kati ya watu ambao wanaonekana kukwamisha juhudi za serikali za mtaa huo za kujitolea kuleta maendeleo ya mtaa huku wakimwomba mwenyekiti wao kuliangalia hilo kwa umakini kwani baadhi ya watu wametoa maeneo yao kwa hiyari na ni kwanini mtu mmoja hakwamishe jitihada za watu Wengi.


IMEANDALIWA NA MADUKA ONLINE
Share it:

JOEL MADUKA

habari

Post A Comment:

Also Read

GEITA YAKABIDHI MWENGE WA UHURU MKOANI KAGERA

Mkuu wa Geita,Mhandisi Robert Gabriel akimkabidhi mwenge wa uhuru Mkuu wa mkoa wa Kagera, Meja Jenerali Mstaafu Salum

JOEL MADUKA