TUME YA UTUMISHI WA WALIMU YATAJWA KUONGEZA UBORA SEKTA YA ELIMU

Share it:


Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mkoani Dodoma Mhe. Deogratius Ndejembi akisisitiza jambo alipokutana na ujumbe wa Tume ya Utumishi wa Walimu ulipotembelea Wilaya hiyo mapema leo ukiongozwa na Mkuu wa Kitengo cha TEHAMA wa Tume hiyo Bi. Devotha Gabriel.
Mkuu wa Kitengo cha TEHAMA kutoka Tume ya Utumishi wa Walimu  akimuonesha Katibu Msaidizi wa Tume ya Utumishi wa Walimu Wilaya ya Kongwa Mkoani Dodoma Bw. Edward  Chamwela namna ya kutumia mfumo rasmi wa barua pepe za Serikali (GMS) ili kuimarisha Mawasiliano ngazi ya Wilaya na Taifa.




Mkuu wa Kitengo cha TEHAMA kutoka Tume ya Utumishi wa Walimu  akimuonesha Katibu Msaidizi wa Tume ya Utumishi wa Walimu Wilaya ya Kongwa Mkoani Dodoma Bw. Edward  Chamwela namna ya kutumia mfumo rasmi wa barua pepe za Serikali (GMS) ili kuimarisha Mawasiliano ngazi ya Wilaya na Taifa.



(Picha zote na Frank Mvungi- MAELEZO Dodoma)




Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) imetajwa kuwa kiungo muhimu katika kuwawezesha walimu kutoa mchango wao utakaosaidia kukuza Kiwango cha elimu hapa nchini.

Akizungumza wakati wa ziara ya Ujumbe wa Tume hiyo Wilayani Kongwa Mkoani Dodoma Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe. Deogratius Ndejembi amesema kuwa anaipongeza Tume hiyo kwa kuweka mkazo katika matumizi ya TEHAMA.

“Teknolojia ni jambo muhimu sana katika kusaidia kuharakisha maendeleo na kuongeza ufanisi kwa kuondoa udanganyifu unaoweza kujitokeza katika kutekeleza majukumu mbalimbali ya kuwahudumia wananchi “ Alisisitiza Ndejembi
A
kifafanua  zaidi Mhe. Ndejembi amesema mifumo ya TEHAMA inayoenda sambamba na mahitaji ya ulimwengu wa sasa ni chachu ya maendeleo hapa nchini.

Kwa upande wake Katibu Tawala wa Wilaya hiyo Bw. Audiphace Mushi amesema kuwa Tume imewezesha walimu kutambua haki na wajibu wao,kusaidia walimu kupata haki zao kwa wakati.

Tume ya utumishi wa Walimu imekuwa mhimili muhimu katika kuwasimamia walimu hivyo ni vyema kila mdau akasaidia juhudi za Tume ili kuimarisha utendaji wake.

Tume ya Utumishi wa Walimu imetembelea Wilaya za Chemba, Bahi, Chamwino,Kondoa, Mpwapwa na Kongwa ili kujionea hali halisi ya utendaji wa Makatibu Wasaidizi wa Tume ngazi ya Wilaya hali itakayochochea na kuhamasisha wadau kujitokeza na Kusaidia Tume kukabiliana na changamoto zinazowakabili walimu kote nchini.


  


Share it:

habari

Post A Comment: