 |
Meneja mkuu wa mgodi wa Bulyanhulu Bernedict
Busunzu akipatiwa maelezo na mkurugenzi wa Read International ,Bi Magdalena George wakati walipokuwa wakitembelea maktaba ya jamii ambayo hipo wilayani Nyang’hwale ,katika kati ni katibu tawala wa Wilaya hiyo Fabian Sospeter. |
 |
Meneja mkuu wa mgodi wa Bulyanhulu Bernedict
Busunzu akikata utepe na katibu tawala wa Wilaya ya Nyang’hwale Bw,Fabian Sospeter wakati wa zoezi la kukabidhi maktaba hiyo. |
 |
Sehemu ya vitabu ndani ya maktaba ya jamii wilayani Humo. |
 |
Sehemu ya vitabu ndani ya maktaba ya jamii wilayani Humo. |
|
 |
Meneja Ufanisi wa mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu,Bw Elias Kasititila akielezea namna ambavyo wameguswa kuchangia maktaba hiyo. |
 |
Bi,Vannesa Kasoga akisoma taarifa ya ukamilikaji wa maktaba hiyo tangu ilipoanza kufanyiwa maboresho na kampuni ya ACACIA. |
 |
Mkurugenzi wa Read International ,Bi Magdalena George akielezea namna ambavyo wameweza kufanukisha kuhakikisha maktaba inakuwa kwenye muonekano bora. |
 |
Katibu tawala wa Wilaya ya Nyang’hwale Bw,Fabian Sospeter akiwasisitiza wananchi pamoja na wanafunzi kutumia maktaba hiyo kujifunza mambo mbali mbali. |
 |
Meneja mkuu wa mgodi wa Bulyanhulu Bernedict
Busunzu akizungumza na wananchi pamoja na wanafunzi wakati wa zoezi la kukabidhi na kuzindua maktaba ya jamii wilayani Nyang’hwale. |
 |
Wananchi ambao wamejitokeza kwenye zoezi la uzinduzi wa Maktaba. |
 |
Wanafunzi wa shule ya Msingi Karumwa wakiwa kwenye uzinduzi wa maktaba ya jamii. |
Na,Joel Maduka.
Mgodi wa
acacia Bulyanhulu kwa kushirikiana na shirika lisilo la kiserikali la read international wamekabidhi maktaba ya
kisasa ya jamii ambayo imetumia kiasi cha sh,milioni 23 hadi kukamilika kwake kwa halmashauri ya wilaya ya Nyang’hwale
ambayo itawasaidia wananchi kupata maarifa na kujifunza mambo mbali mbali
kutokana na vitabu ambavyo vinapatikana.
Akizungumza wakati wa shughuli ya kukabidhi wa maktaba ya jamii,meneja mkuu wa mgodi wa Bulyanhulu
Bernedict Busunzu alisema kuwa wanaamini katika kufikia Tanzania ya viwanda
basi ni vyema watu wakawa na ufahamu ambao utawasaidia kujua fursa mbali mbali
ambazo zinawazunguka hivyo kupitia maktaba hiyo wananchi wanaweza kusoma vitabu
ambavyo vitawasaidia kujua mambo mbali mbali.
“Tunatambua
umuhimu wa elimu na tunaimani kuwa jamii ya Wilayah ii itatumia vyema Maktaba
hii kwa kusoma na pia kujifunza mambo mbali mbali ambayo yamo kwenye vitabu
ambavyo vipo kwenye maktaba hii hivyo tunaomba iweze kutunza kama vile sisi
tulivyoikabidhi ikiwa katika hali nzuri”Alisema Busunzu.
Hata hivyo
kwa upande wake Katibu Tawala wa wilaya Hiyo Fabian Sospeter aliwataka wananchi pamoja na wanafunzi kujenga desturi
ya kupenda kusoma vitabu mara kwa mara
na kwamba kufanya hivyo wataweza kujua mambo mengi zaidi.
“Wananchi
niwasisitize kutumia maktaba hii kujifunza na kusoma masuala mbali mbali na
ndani ya maktaba hii kuna vitabu vya kilimo ambavyo vitawasaidia wakulima
kulima kilimo cha kisasa na ambacho kitawaletea faida”Alisema Fabian
Bw Mabura
Makonga na Georgi John walisema kuwa wanaamini kuwa maktaba hiyo itawasaidia
kujua mambo mbali mbali huku wakishauri elimu itolewa zaidi kwa wananchi
kutambua umuhimu wa kujenga tabia ya
kupenda kujisomea kwani wengi wao awana elimu na jambo hilo ni geni kwenye
Wilaya hiyo.
Hata hivyo
Bi,Vannesa Kasoga ameelezea uhaba ambao wanao kwenye maktaba hiyo kuwa ni upungufu wa kompyuta saba,mashine ya
kuzalisha nakala na upungufu wa baadhi ya vitabu.
Post A Comment: