CCM WAFUNGA KAMPENI KWA KISHINDO KATA YA SENGA

Share it:
Mbunge wa Jimbo la Geita,Joseph Msukuma na Mbunge wa Geita Mjini,Constatine Kanyasu wakiwa na Mgombea udiwani wa kata hiyo wakati walipokuwa wakielekea kwenye ofisi za chama hicho kijiji cha Senga.
Mamia ya wananchi  waliohudhulia Mkutano huo wakimsikiliza Mbunge wa jimbo la Geita.Joseph Msukuma.









Na,Consolata Evarist ,Geita

Chama cha mapinduzi(CCM)Wilaya  ya Geita kimefunga kampeni zake za kumnadi mgombea udiwani wa kata ya Senga,huku kikiahidi kuendelea kutekeleza na kutatua matatizo ya wananchi kwenye kata hiyo.


Akimnadi mgombe udiwani wa kata hiyo,Mwenyekiti wa ccm Mkoani humo,ambaye pia ni mbunge wa Jimbo la Geita,Joseph Msukuma,alisema kuwa chama hicho kimeendelea kujidhatiti kwa kutatua  kero mbalimbali  ikiwa ni pamoja na huduma za afya ,miundombinu ya barabara hususani zile za vijijini na umeme.


“Rais Magufuli ametupa lami kilomita  hamsini na saba kutoka Geita kwenda  Nkome bado tu mnaendelea kuchagua upinzani inatakiwa tuwe kimya ili tujengewe  bugando yetu ndugu zangu na niwaombe ndugu zangu tutulie na chama chenu ambacho kinampango mzuri wa kuendeleza maendeleo na sio kuwa na siasa zisizo kuwa na maana nyie wenyewe mnaona wanachama wao wanaama”Alisema Msukuma.


Msukuma  aliendelea kusema kuwa kwasasa wameshaanza kupima ngunzo za umeme na kwamba wanatarajia vijiji vyote kufikia mwakani viwe vimesambaziwa umeme kwenye Mkoa wa Geita.


Aidha Mbunge wa Jimbo la Geita,Mjini Constatine Kanyasu,alisema kuwa kampeni za kutoa ahadi ziliishia mwaka 2015 kwani kwasasa wanaye mbunge ,Rais na kwamba wao kama wananchi wa kata ya Senga ni vyema basi wakahakikisha wanaunganisha nguvu kwa kumchangua kiongozi ambaye anatoka ndani ya chama hicho.


Akiomba kura kwa wananchi mgombea udiwani wa kata hiyo kupitia (CCM),Thomas Tumbo,aliwaahidi wananchi  kushirikiana nao katika utatuzi wa ujenzi wa zahanati,pamoja na vyumba vya madarasa ambavyo vimeonekana kuwa ni changamoto kubwa kwenye kata hiyo.

Uchaguzi mdogo wa kata hiyo unatarajia kufanyika jumapili ya  Novemba 26 na vyama vinavyoshiriki ni vitatu,CHADEMA,CUF na CCM.



Share it:

JOEL MADUKA

SIASA

Post A Comment: