Shirikia
lisilo la kiserikali la JSI limetoa Baiskeli 32 na makabati 13 kwa ajili ya
kuendeleza mapambano dhidi ya unyanyasaji wa watoto wanaoishi kwenye mazingira
hatarishi .
Akizungumza
baada ya kugawa Baiskeli hizo kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita,
Mkurugenzi wa JSI kanda ya ziwa Dr Amos Haki Nsheha amesema wilaya hiyo ina
watoto wengi wanaoishi katika mazingira hatarishi.
Alisema
watoto hao wanafikia karibu elfu 20 na kwamba kutokana na mazingira wanayoishi
wana hatari ya kupata maambukizi ya virusi vya ukimwi kutokana na kufanyiwa
vitendo viovu ikiwemo kubakwa.
Afisa ustawi
wa Jamii wa wilaya ya Geita Bw Anderson
Shimbi amesema matukio ya ukatili kwa mwaka jana yalikuwa 97 kutoka kata
37 ambapo wanaume ni 40 na wanawake 57 na kwamba ukatili unaofanywa zaidi ni
vipigo, ubakaji na wengine kutopewa nafasi ya kwenda shule .
Mmoja kati
ya wasimamizi wanaotoa huduma kwa watoto wanaoishi kwenye mazingira hatarishi,
Bw Tom Jarusinga amesema msaada huo umetolewa katika wakati muafaka kwani wengi
wao walikuwa na shida ya usafiri wa kuwafikia watoto wanaofanyiwa ukatili.
Mkurugenzi
wa Halmashauri wa wilaya ya Geita Bw Ali Kidwaka amesema mchango huo utasaidia
kuelekea kwenye malengo ya dunia ya kupambana na ukimwi na kufikia malengo ya
asilimia 90 ya watu wote wenye maambukizi kujua hali zao.
Post A Comment: