VIFO VYA WIVU WA MAPENZI VYADAIWA KURUDISHA NYUMA MAENDELEO GEITA

Share it:
Mkuu wa Mkoa wa Geita,Mhandisi Robert Luhumbi  ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati na ulinzi akizungumza hivi karibuni na waandishi wa habari wakati alipokuwa akitoa taarifa ya Mkoa huo.

 Na,Joel Maduka,Geita
Imeelezwa kuwa vifo vinavyotokana na wivu wa Mapenzi vimekuwa vikichangia kurudisha nyuma maendeleo ya mkoa wa Geita kwa kuwa vinapoteza nguvu kazi ya taifa.

Mkuu wa mkoa wa Geita Mhandisi Robert Luhumbi alisema vifo hiyo vinachangia kurudisha nyuma maendeleo ya mkoa huo kutokana na wengi wao kujichukulia maamuzi ya haraka bila kuwashirikisha baadhi ya watu wanaoweza kuwasaidia kutatua migogoro yao.

Ameyataja baadhi ya matukio makubwa yaliyosababisha watu kufariki katika maeneo mengi ya mkoa huo kuwa ni kujichukulia sheria mkononi, ugomvi wa kuwania mali, ushirikina na wivu wa mapenzi.


Mhandisi Luhumbi ametoa wito kwa viongozi wa madhehebu ya dini kuwashauri na kuwasaidia watu wenye migogoro ya kifamilia ili kuendelea kuuweka mkoa huo katika hali ya usalama 
Share it:

JOEL MADUKA

mapenzi

Post A Comment:

Also Read

HABARI KUBWA KWENYE MAGAZETI YA LEO IJUMAA 25 MAY 2018

JOEL MADUKA