CCM WAKABIDHI MABATI KUKAMILSHA NYUMBA YA MGANGA.

Share it:

Katibu wa Chamaa cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu, Nicholaus Kasendamila akimkabidhi Mabati 74 mtendaji wa kijiji cha Ikungulyandili Magembe Charles (mwenye shati jeupe) kwa ajili ya kupaulia jengo la mganga katika zahanati ya kijiji hicho, kushoto ni Diwani wa viti maalumu kata ya nkololo Juliana Itabaja.


Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Nicholaus Kasendamila akimpokea Mwenyekiti wa kijiji cha Mwasilimbi Ng'ombe Ntemi baada ya kuhamia CCm kutoka Chadema na kukimvisha kofia na bendera ya CCM, kama ishara  ya kupokelewa.

Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Nicholaus Kasendamila akimpokea Mwenyekiti wa Kitongoji cha Mwakitwala-Ihusi Kishili Ndongio baada ya kuhama kutoka Chadema kuja CCM na kumvisha kofia na bendera ya chama kama ishara ya kupokelewa rasmi. (PICHA ZOTE NA COSTANTINE MATHIAS).
NA COSTANTINE MATHIAS, BARIADI.

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu kimekabidhi mabati 74 yenye thamani zaidi ya shilingi 900,000 kwa ajili ya kupaulia nyumba ya Mganga katika zahanati ya Ikungulyandili.

Akikabidhi msaada huo, Katibu wa CCM wilayani hapa Nicholaus Kasendamila alisema kuwa wanatoa mchango huo ili kukamilisha ujenzi na pia kuunga mkono nguvu za wananchi waliojenga boma la nyumba hiyo.

Kasendamila aliwataka viongozi wa kijiji hicho kuyatumia ipasavyo mabati hayo kama yalivyoelekezwa, huku akisisitiza juu ya usimamizi wa rasilimali za chama na za serikali.

‘’baadhi ya viongozi wa chama na serikali wamekuwa wakihujumu mali za chama kwa kuona kuwa hazina msimamizi…lakini niwaombe kwa yeyote aliyehujumu mali ya chama hatutasita kumchukulia hatua’’ alisema Kasendamila.


Akiongea mara baada ya kupokea mabati hayo, Mtendaji wa kijiji hicho Magembe Charles alimhakikishia katibu huyo kuwa baada ya siku tatu, watakuwa wamekamilisha kupaua jengo hilo kwa sababu wameshapandisha kenchi na vifaa vingine vipo.

Katika hatua nyingine chama hicho kimepokea wanachama wawili ambao ni mwenyekiti wa kijiji cha Mwasilimbi-Ihusi na Mwenyekiti wa Kitongoji cha Mwakitwala-Ihusi waliohama kutoka chadema kurudi CCM.

Wakiongea mara baada ya kukabidhi kadi zao walisema kuwa awali walishawishiwa na baadhi ya watu, lakini kwa sasa wamekuwa hawana msaada kwao wakiwafananisha Chadema na mwindaji aliyeenda porini na kumwacha mbwa awinde bila kumsaidia.

‘’ nimeona chama kimepoteza mwelekeo na hakipo…sawa na mtu aliyesindikiza mbwa kwenda kuwinda halafu yeye akarudi kulala, nimeamua kuhama mwenyewe na wala sijashinikizwa na mtu yeyote’’ alisema Ng’ombe Ntemi aliyekuwa Mwenyekiti wa kijiji cha Mwasilimbi.


Share it:

JOEL MADUKA

SIASA

Post A Comment:

Also Read

WATUMISHI 7 WAFUKUZWA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA.

Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Geita,Elisha Lupuga akitangaza hatua zidi ya watumishi saba ambao wamekutwa na

JOEL MADUKA