BODA BODA WASIOVAA KOFIA NGUMU (ELEMENT) GEITA KUKAMATWA

Share it:
Mhandisi Robert Gabriel Mkuu wa Mkoa wa Geita aliyevaa  koti la rangi ya dhambarau na miwani akipata maelezo juu ya matumizi ya kamera za barabarani kutoka kwa Inspekta wa Usalama barabarani Mkoa wa Geita Mark Thomas Masawe wakati wa ukaguzi wa mabanda ya maonyesho katika maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani Mkoani Geita.

 Mtaalam wa Mamlaka ya udhibiti wa usafiri wa nchi kavu na Majini (SUMATRA) ndugu Hagai Ruben akitoa maelezo kuhusu ukataji wa leseni za usafirishaji kwa Mkuu wa Mkoa wa Geita Robert Gabriel wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama barabarani iliyofanyika kimkoa Katoro Geita.
Wataalam wa Jeshi la Zima Moto na Wokozi Mkoa wa Geita wakieleza mbele ya wajumbe wa baraza la usalama barabarani  Mkoa wa Geita matumizi mbalimbali ya mitungi yenye Gesi ya kuzima moto baada ya kamati hiyo kutembelea banda la kikosi hicho.


Ndugu Emmanuel Chacha mtaalam kutoka kampuni ya uchimbaji wa madini Geita (GGML) akitoa ufafanuzi  kwa Mkuu wa Mkoa wa Geita na wajumbe wa baraza la Usalama barabarani kuhusu matumizi ya vifaa vya wokozi katika maeneo ya migodi.

Wanafunzi wa Shule za Msingi za Mji wa mdogo wa Katoro wakiwa katika maandamano ya maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama barabarani Mkoani Geita.

Maandamano ya maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa usalama barabarani yakipita mbele ya Mgeni rasmi (hayupo kwenye picha).

Waendesha Piki Piki maarufu kama boda boda wakiwa katika maandamano ya maadhimisho ya wiki ya nenda kwa usalama barabarani iliyofanyika Katoro Geita.

Mhandisi Robert Gabriel Mkuu wa Mkoa Geita akimpongeza ndugu Alfred Hussein Mkuu wa Kikosi cha Usalama barabarani Mkoa wa Geita wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama barabarani Mkoani Geita.

Mkuu wa Mkoa wa Geita Robert Gabriel akihutubia wananchi(awapo katika Picha) wakati wa wa uzinduzi wa maadhimisho ya Wiki ya nenda kwa Usalama barabarani Mkoani Geita.


Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel Luhumbi amemuagiza Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani  Mkoa wa Geita Alfred Hussein kuwakamata na kuwafikisha katika vyombo vya sheria waendesha pikipiki wote wasiovaa kofia ngumu maarufu kama element wanapotimiza majukumu yao ya usafirishaji wa abiria.

Akizungumza katika uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya nenda kwa usalama barabarani ambayo kimkoa yanafanyika Mji mdogo wa Katoro Wilaya ya Geita Mheshimiwa Robert Gabriel amesema muendesha piki piki yeyeto asiyevaa kofia ngumu Mkoani humu  akamatwe na kuwekwa ndani ili liwe fundisho kwa watu wote wasiopenda kutii sheria na matokeo yake wanasababisha vifo kwa jamii. 
"Naamini kuanzia wakati huu RTO na Kamati za Usalama barabarani Mkoa na Wilaya mtu asiyevaa kofia ngumu atakamatwa na kuwekwa ndani tutatumia sheria zote hakuna kupatana hakuna kuelewana". Ameongeza kuwa watumiaji wa vyombo vya moto wanatakiwa kuelimishwa na kufundishwa taratibu zinazowaongoza katika utumiaji wa vyombo hivyo na kuwataka wananchi kujitokeza kwa wingi pamoja na vyombo vyao wapate elimu ili kujua mbinu za kuwafanya kuwa salama.

Mhandisi Robert Gabriel amewataka abiria kutoa taarifa kwa vyombo vya usalama pamoja na kutowaruhusu madereva kuendesha vyombo vya moto kwa mwendo kasi kwa kuwa jukumu la Usalama ni la kila mwananchi.

Aidha, amekipongeza kikosi cha usalama barabarani mkoani hapa kwa kazi nzuri ya kuzingatia usalama wa wananchi katika barabara,  amewataka waendelee kusimamia suala hili na kuchukua hatua pale inapobidi.

Awali Mkuu wa Kikosi cha usalama barabarani mkoani hapa ndugu Alfred Hussein alimweleza Mkuu wa Mkoa kuwa kuwa ajali za barabarani zimepungua kutoka ajali 87 mwaka 2016 hadi kufikia ajali 68 kwa mwaka huu. Vile vile ameeleza kuwa idadi ya vifo pia imepungua kutoka vifo 98 mwaka 2016 hadi vifo 79 kwa mwaka huu wa 2017.

 Alfred ameongeza kuwa kwa ajali nyingi zinasababishwa madereva kuendesha vyombo vya moto wakiwa wametumia vilevi mbalimbali, mwendo kasi, kukosa umakini barabarani, uchakavu wa vyombo vya usafiri na miundombinu.  Maadhimisho haya yanafanyika kwa wiki nzima ambapo wananchi, madereva na wamiliki wa vyombo vya moto wanapata elimu kwa lengo la kuhakikisha kila mtu anajikinga na ajali za barabarani.

Share it:

JOEL MADUKA

habari

Post A Comment:

Also Read

JECHA ANG'ATUKA TUME YA UCHAGUZI ZANZIBAR

Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) Jecha Salim Jecha amemaliza muda wake wa majukumu ya tume hiyo kwa ki

JOEL MADUKA