KANGI LUGOLA AITAKA KAMPUNI YA GGM KUWALIPA FIDIA WANANCHI AMBAO WAMO NDANI YA ENEO LA MGODI

Share it:
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh.Kangi Lugola akitoa maelekezo kwa mgodi wa dhahabu wa Geita(GGM)mbele ya wananchi ambao walikuwa wamekusanyika kumsikiliza.

Wananchi  wa Katoma wakimsikiliza Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh.Kangi Lugola wakati alipokuwa akitoa maagizo.


Na,Consolata Evarist,Geita

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh.Kangi Lugola ameutaka mgodi wa dhahabu wa Geita(GGM) kuwalipa fidia wananchi ambao wapo ndani ya mgodi huo ndani ya mwezi mmoja,huku akiwapiga faini ya milioni Kumi kutokana na uharibifu wa mazingira.

Alisema mgodi huo  umeonekana kuwa nje ya kiwango cha kipimo ambacho kinaonesha  vumbi linalotoka linaathari  kwa wananchi  na kwamba  kutokana  kosa hilo mgodi umeadhibiwa kulipa faini ya shilingi Milioni kumi ili kuendelea kulinda afya za watanzania .

Kangi ameendelea kusema kwamba serikali ya Rais Magufuli  haipo tayari  kuona watu wake wanafanyiwa majaribio kwa kuwavunjwa sheria ambazo zimewekwa kwaajili ya kuendelea kuyatunza na kuyahifadhi mazingira.

Kuhusu suala la fidia Naibu waziri ameutaka mgodi wa GGM pamoja na serikali Mkoani Geita kuhakikisha wananchi ambao wapo ndani ya mgodi wawe wamelipa fidia wale ambao wanazunguka maeneo hayo na kuwataka wamalize tatizo la kimazingira.

Diwani wa kata ya Kalangalala Sospeter Mahushi alisema wananchi wameendelea kukosa amani na furaha na kwamba ni vyema sasa serikali ikatoa tamko  kama waendeleze makazi yao au GGM iwafidie waweze kupisha maeneo hayo kwani wamekuwa wakipata shida pindi milipuko inapotokea hali ambayo imekuwa ikiwaradhimu wengi wao kukimbia makazi wakati wa shughuli za ulipuaji wa miamba.


Bi ,Elizabert  Charles ambaye ni mkazi wa mtaa wa Katoma   alitoa  malalamiko  na kudai amepata matatizo ya kiafya kutokana na milipuko ambayo imekuwa ikifanywa na mgodi wa Geita (GGM )na  kwamba hakutendewa haki ya kimatibabu na ameathirika.
Share it:

JOEL MADUKA

habari

Post A Comment:

Also Read

HABARI KUBWA KWENYE MAGAZETI YA LEO IJUMAA APRILI 20, 2018

JOEL MADUKA