
Upendo Peneza amekanusha uvumi kuwa anampango wa kuhamia Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Kwamujibu wa Peneza amesema hana sababu za kuhama chama chake na amewashangaa wabunge wanaofanya hivyo.
Peneza pia amewataka wananchi kutowachagua wabunge ambao wamejiuzulu hivi karibuni kama watarudi kuwaomba kura kupitia vyama vyao vipya.
“Nachukizwa na uvumi huu nachukizwa na tabia hii ya watu kujiuzulu katikati ya safari na kuwaongezea wananchi gharama ya nyongeza,” amesema Peneza.
Mbunge huyo amewataka wabunge wenzie waunge mkono mazuri na kupinga mabaya ndani ya vyama vyao na wakumbuke kuwa waliomba ridhaa za wananchi na kodi zao ndizo zilizowafikisha walipo.
Post A Comment: