Waziri wa nishati,Dkt Medard Kalemani amewaakikishia
wananchi wa kata ya Bulega Wilayani
Bukombe Mkoani Geita kwamba kila kijiji
kitahakikisha kinafikiwa na mradi wa umeme wa REA na kwamba watakapoanza kuweka
mitambo kwenye vijiji hakuna nyumba ambayo itaweza kurukwa watahakikisha zote
zinafikiwa na mradi huo.
Kalemani ameyasema hayo wakati alipokuwa kwenye ziara ya
kikazi ya kukagua uwekaji wa umeme wa REA awamu ya tatu ambao unatarajia
kuchukua miaka miwili ili kukamilisha zoezi hilo kwa maeneo yote ya vijijini.
Waziri Dk Kalemani
amesema katika awamu ya kwanza na ya pili ya Mradi wa REA wilaya ya Bukombe
haikuwepo lakini kwa awamu ya tatu wamefaidika na Vijiji 70 vimeingizwa katika
mpango na ifikapo januari 12 mwakani umeme utakua tayari umewaka.
kuwa kwa maeneo ya vijiji vya Bukombe mkandarasi
amesha jiandaa kufikisha nguzo tarehe 15 mwezi January mwaka 2018.
Naye Mbunge wa Jimbo la Bukombe Doto Biteko amewataka
wananchi ambapo umeme utakuwa umefika
kwenye vijiji vya kutumia fursa hiyo kujinufaisha ikiwemo kufungua miradi
ambayo itakuwa inatumia nishati hiyo.
Huku akiwasisitiza wananchi hao kuendelea kumuunga mkono
Rais Magufuli kutokana na shughuli
ambazo anazifanya likiwemo suala la kuleta nidhamu kwenye taasisi mbali mbali
za serikali.
Post A Comment: