WACHINA WAWILI WAFARIKI MGODINI

Share it:



Raia wawili wa Nchini China wamefariki Dunia wakati wakiwa ndani ya shimo lenye kina cha Urefu wa zaidi ya mita 100 wakati wakifanya kazi ya kulipua miamba yenye dhahabu mkoani Geita.

Akizungumza na waandishi wa habari kamanda wa polisi Mkoani Geita ,Mponjoli  Mwabulambo, alisema mnamo 20Mwezi wa tatu(3)  saa tatu na dakika arobaini usiku, raia hao walifikwa na umauti wakiwa katika kijiji cha Nyamtondo ndani ya mgodi unao milikiwa na Mayala  Ngweso, mfanyabiashara wa madini katika mgodi wenye PML No.0001333, ulio na ubia na kampuni ya kichina iitwayo TAICHANGAIN  TANZANIA GROUP katika Kata ya Kaseme  tarafa ya Butundwe  wilaya na mkoa wa Geita.

Kamanda ameeleza chanzo cha ajali hiyo ni uzembe uliofanyika na kupelekea kulipukiwa na mlipuko wakati wakiwa ndani ya shimo na kusababisha majeraha makubwa kwenye miili yao ambayo yalipelekea vifo vya raia hao.

Amewataja Raia hao ambao ni Bw,Li-Shaobin,{44}, mwenye passipot No 6796105 ,ambae amepata majeraha makubwa kisogoni, na Bwn,Qian Zhaorang, {49}, mwenye passipoti  No 5834285,ambae amepata majeraha makubwa kichwani na kuvunjika mguu wa kulia.

Amesema miili yao imefanyiwa uchunguzi na daktari mnamo 24 machi  mbele ya Shann  Ly,{29} mwenye Paspoti No E.5968863 ambae ni site Meneja, miili yao iliihidhiwa katika chumba cha maiti katika hospitali ya Makoye iliopo Geita.

Pia ameongeza kwa kusema hawawezi kumshikilia mtu yoyote kutokana na ajali hii kwani uchunguzi umeonesha chanzo cha ajali hiyo ni uzembe wao na kutochukua tahadhari kabala ya kuanza shughuli zao.

Kamanda hiyo ametoa rai kwa wachimbaji wote kuchukua tahathari pale wanapofanya shughuli za uchimbaji ili kuepuka ajali zinazoweza kuepukika.

Share it:

JOEL MADUKA

habari

Post A Comment:

Also Read

MWALIMU AKAMATWA KWA KUJIHUSISHA KIMAPENZI NA MWANAFUNZI WAKE

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita,Mponjoli Mwabulambo akifafanua juu ya hatua ambazo wamezichukua kwa mwalimu N

JOEL MADUKA