WANACHUO WAPEWA FEDHA GEITA.

Share it:
Wanachuo wakiwawakiwa katika makundi makundi wakisubili kujua mwafaka wa pesa zao.

Wakifatilia kwa makini kikao na mkuu wa wilaya.

Mkuu wa chuo ambae anatuhumiwa kula pesa za wanafunzi,mwalimu Sindano Masanja.

Mkuu wa Wilaya ya Geita Herman Kapufi,akitoa maagizo juu ya malipo ya wanachuo wa rich rice

Nyaraka za siri za serikali zilizokutwa kwenye ofisi ya mkuu wa chuo.

mkaguzi msaidizi wa jeshi la polisi,Tungalaza George,akitoa ufafanuzi juu ya uchunguzi waliofanya.

Kaimu mkurugenzi wa chuo hicho Bahati charles

Mhasibu na mtaaluma wakiwa chini ya ulinzi.

Wanachuo wakiteta jambo na Mkuu wa wilaya.

Walio jaribu kutorosha fedha wakiwa wamekamatwa na kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya.


Wanafunzi wakisubilia malipo yao.

GEITA:Kaimu mkuu wa mkoa wa  geita ambaye ni mkuu wa wilaya ya geita hermani kapufi ameamuru kuwekwa   ndani kwa aliyekuwa mkuu wa chuo cha ualimu geita cha rich rise,mhasibu na mkurugenzi wa chuo hicho baada ya kushindwa kurejesha ada za wananchuo wapatao 300  wa mwaka wa kwanza kiasi cha milioni 230 .

Hatu hiyo ya kutaka kurejeshewa fedha zao imejiri baada  ya uongozi wa chuo hicho kuendelea kudai kuwa wanafunzi wa mwaka wa kwanza kozi ya ualimu wa chakechea yani  ecde ambayo  kwa sasa haitambuliwi na baraza la mitihani la taifa necta kutokana na kufutwa .

Akitoa maelezo kwa kaimu mkuu wa mkoa,kaimu mkurugenzi wa chuo hicho Bahati charles,alimwomba  mkuu wa mkoa kuwaomba wanafunzi wapokee kiasi cha sh,milioni115   huku wakiendelea kutafuta pesa zingine za kutoa fidia kwa wanafunzi hao.

“Zoezi la kwanza ndungu mkuu wa mkoa uliagiza tuwapatie vyeti zoezi hilo tumeshakamilisha kwa asilimia tisini zoezi la pili ni kuhusu pesa tatizo kubwa lililokuwepo hapa ni kuanzisha kozi ya ECDE ambayo hipo kinyume na taratibu kutokana na kuagiza vijana wote wapewe pesa zao uwangozi wa chuo umeandaa nusu ya pesa ambayo watalipwa vijana na pesa itakayobakia watalipwa kwa awamu nyingine”alisema Charles

Hata hivyo kwa upande wake, mkaguzi msaidizi wa jeshi la polisi,Tungalaza George,alisema kuwa wamefanya ukaguzi katika ofisi ya mkuu wa chuo hicho na kubaini kuwa kuna nyara za siri za serikali zimetumika zisivyo kwani kunamitihani ya Taifa ambayo inatakiwa kuwa Necta imekutwa ikiwa ndani ya ofisi.

Baada ya maelezo hayo mkuu wa wilaya ambae pia ni kaimu mkuu wa mkoa wa Geita,Herman Kapufi,alitoa maagizo ya kukamatwa kwa mkurugenzi na mhasibu na mkuu wa chuo aliyekuwapo chuoni hapo kipindi cha nyuma,Sindano Masanja.

“Na kwasababu tumefikia katika hatua hii  na taarifa niliyohipata ni kwamba kuna milioni 115 haya kama ni milioni 115  maelekezo yangu ni kama ifatavyo mmiriki wa chuo,mhasibu,mwalimu wa taaluma Ruben Kubwa ,meneja wa shule naomba mkae pale chini ya ulinzi paka zipatikane hizo fedha.”alisema Kapufi.

Baadhi ya wanachuo chuoni hapo wamepongeza uwamuzi huo wa kaimu mkuu wa mkoa wakiamini kuwa watapatiwa haki zao ambazo walikuwa wakidai,lakini pia wamelalamika kwa kusoma kozi hewa ambayo imeshafutwa muda mrefu.

Mkuu huyo amesema wanachuo hao wasiondoke chuoni hapo mpaka watakapopewa fedha zao zote na mala baada ya   kulipa fedha hizo viongozi watachukuliwa hatua kwa makosa madogo ambayo yamejitokeza chuoni hapo.

Lakini katika hali isiyo ya kawaida baadhi ya watumishi chuoni hapo walionesha kukiuka agizo la DC na kutaka kutorosha fedha ambazo zilitakiwa kugawiwa wanafunzi lakini hata hivyo awakufanikishwa kwani kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ilikuwa macho na mwisho wa siku waliwekwa chini ya ulinzi kwa kosa la kujaribu kutaka kutorosha fedha hizo.


Imeandaliwa na Joel Maduka

Share it:

habari

Post A Comment: