WAHANGA 15 WALIONUSURIKA NA KIFO BAADA YA KUFUKIWA GEITA WAMERUHUSIWA KUTOKA HOSPITALI

Share it:
Mkuu wa Mkoa wa Geita Meja Jenerali Mstaafu,Ezekiel Kyunga akiwasalimia wachimbaji ambao walikuwa wamefukiwa na kifusi kwenye Mgodi wa RZ,katika Hosptali ya Rufaa ya Geita.

Mkuu wa Mkoa wa Geita Meja Jenerali Mstaafu,Ezekiel Kyunga,akitaniana na wachimbaji hao.


Mkuu wa Mkoa wa Geita Meja Jenerali Mstaafu,Ezekiel Kyunga,akiendelea kusalimiana na wananchi na hapa ni raia wa kichina.

Mchungaji wa kanisa la FPCT Geita Mathias Gundula  ,Akimshukuru Mungu juu ya yale ambayo ameyateda kwa vijana ambao wameokolewa kutoka mgodini.

Mganga mfawidhi wa Hospital ya mkoa wa Geita Dk. Brian Mawalla akimwakikishia mkuu wa mkoa kuwa vijana wapo salama na wanaweza kwenda kuendelea na majukumu ya ujenzi wa Taifa

Mwanasheria wa mgodi huo,Francis Kiganga,akimwakikishia mkuu wa mkoa kutekeleza maagizo yote ambayo wamepatiwa. 
Mwanasheria wa mgodi huo,Francis Kiganga akionesha ramani ya shimo mbele ya waandishi wa habari wa vyombo mbali mbali.

Moja kati ya waanga wa tukio hilo akimshukuru Mkuu wa Mkoa kwa jitihada ambazo zimefanyika na wao kutoka wakiwa hai.


Wahanga  15 wakiwemo watanzania 14 na raia mmoja wa kichina  walionusurika na  kifo baada ya kuokolewa kutoka chini ya ardhi kwenye  mgodi wa dhahabu wa RZ union ulioko  kijiji cha mawemeru  kata ya Nyarugusu mkoani Geita baada ya kukaa siku 3 bila chakula wala huduma yoyote wameruhusiwa kutoka Hospital ya mkoa wa Geita walikopelekwa kupata matibabu.

Akiwaaga baada ya kuruhusiwa kutoka hospitari Mkuu wa Mkoa wa huo,Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Kyunga,amewaomba kurudi na kuendelea kujituma katika shughuli ambazo wanafanya  ili kuendelea na ujenzi wa Taifa.

“Mko imara sasa mrudi mkaendelee tena na ujenzi wa Taifa letu shughuli hizi ndio zitawasaidia kupata kipato tumefarijka sana miongoni mwenu hayupo hata  mmoja aliyeteteleka”Alisema Kyunga.

Hata hivyo Mkuu wa wilaya ya Geita,Mwl Herman Kapufi,amesema kuwa wamekubaliana na mgodi huo wafanyakazi wote katika mgodi huo kupatiwa mkataba ambao utawasaidia wafanyakazi na pia amewaomba kuwa na mahusiano baina ya wafanyakazi na Waajili ambo ni Raia wa china na pia amewasisitiza kumrudia Mungu kwani amewanusuru na kifo.

Aidha kwa upande wake Mwanasheria wa mgodi huo,Francis Kiganga pamoja na kuwashuru mashirika ambayo yamejitolea kufanya shughuli za uokoaji pia amemwakikishia mkuu wa wilaya kuongeza mkataba wa kazi badala ya miezi mitatu hatawapa wa mwaka mzima.


Akiwaruhusu wahanga hao, mganga mfawidhi wa Hospital ya mkoa wa Geita Dk. Brian Mawalla amesema wamefikia uamuzi wa kuwaruhusu baada ya kujiridhisha na maendeleo mazuri ya afya zao.


Wahanga hao Wameokolewa January 29 mwaka huu kwa msaada kutoka makampuni ya Busolwa Mining,Nyarugusu,GGM na ACACIA wamefanikiwa kuwaokoa watu hao waliofukiwa na udongo wa kifusi cha mgodi huo Januari 26 mwaka huu.

IMEANDALIWA NA MADUKAONLINE
Share it:

habari

Post A Comment: