Wananchi wa Kijiji cha Nyamtondo Kata ya Kaseme Wilaya
na Mkoa wa Geita Wamesikitishwa na
kitendo cha mwekezaji wa Mgodi wa Nyamahuna
unao milikiwa na Albert Ruzika kushindwa kutekeleza agizo la serikali la
kujenga visima vitatu vya maji kijijini hapo.
Hatua Hiyo imekuja ni baada wa Mkuu wa Wilaya
ya Geita,Mwl Herman Kapufi kutoa agizo la kujenga visima hivyo mwaka jana mwezi wa kumi na mbili
na kwamba kufikia tarehe thelathini mwezi wa tano mwaka huu wawe wamekamilisha
ujenzi huo.
Akizungumza kwenye Mkutoni wa wananchi Diwani
wa Kata ya Kaseme Andrea Kalamla amesema kuwa hadi sasa kuna kisima kimoja tu
ambacho kimejengwa na chenyewe hakitoi maji hadi sasa hali ambayo imekuwa
ikisababisha wanakijiji kutembea umbali mrefu kufuata maji.
“Mkuu wa
Wilaya ungekuwa umefika mapema tungekupeleka kwenye kisima ambacho kimejengwa
ambacho hakina ubora wowote kabisa kwani tunavyozungumza hadi sasa kisima
kimekauka na hakina maji kabisa na mimi kila ninapofika hapa wanakijiji wamekuwa wakiniomba maji hali
ambayo imeendelea kuninyima amani”Alisema Kalamla.
Kwa upande
wake meneja wa mgodi wa huo ,BW Simion Lubamba ameelezea kuwa utekelezaji wa
ahadi za mgodi kwa wananchi zilikwama kutokana na uzalishaji kupungua hivyo amewaomba
wananchi kumpa muda wa miezi miwili atakuwa ametekeleza ahadi hiyo.
“Kweli uhaba
wa maji upo hapa kulingana na agizo lako ambalo uliliandika mwekezaji nilimpa
nakala kwamba anatakiwa kutekeleza ahadi hiyo mwezi wa tano tarehe thelathini
awe ametekeleza lakini alijibu kuwa hali ilikuwa ni mbaya hivyo ameomba kwa
wananchi wampe miezi miwili hatakuwa atahakikisha anatekeleza ahadi
hiyo”Alisema Lubamba.
Kutokana na
maelezo hayo Mkuu wa Wilaya Mwl Herman Kapufi akatoa maagizo kwa afisa madini
juu kufungia mgodi huo hadi pale utakapo tekeleza ahadi yake huku mkuu wa jeshi
la polisi wilayani hapo akitakiwa kuweka
ulinzi wa kutosha .
Wanakijiji
wa kijiji hicho wamepongeza kwa hatua ambayo ameichukua Mkuu wa Wilaya huku
wakidai ni bora wote wakakoswa.
Akizungumzia
Sheria ya madini kuhusu wawekezaji Afisa madini wa Mkoa wa Geita,Ally Said Ally
amesema kuwa mwekezaji anapaswa kutoa huduma za kijamii .
IMEANDALIWA NA MADUKA ONLINE
.
Post A Comment: