SERIKALI GEITA YAFUNGA MGODI WA NYAMAHUNA.

Share it:
Mkuu wa Wilaya ya Geita,Mwl Herman Kapufi akitoa maagizo kwa afisa Madini wa Mkoa wa Geita na Mkuu wa Polisi Wilayani humo wakati wa Mkutano wa hadhara 
Wananchi wakishangalia baada ya maagizo kutolewa.

Viongozi wa Mgodi wa Nyamahuna.


Editha Mathias akizungumza na waandishi wa habari juu ya hatua  ambayo imechukuliwa na Mkuu wa Wilaya.



Wananchi  wa Kijiji cha Nyamtondo Kata ya Kaseme Wilaya na Mkoa wa Geita  Wamesikitishwa na kitendo cha mwekezaji wa Mgodi wa Nyamahuna  unao milikiwa na  Albert  Ruzika kushindwa kutekeleza agizo la serikali la kujenga visima vitatu vya maji kijijini hapo.

Hatua Hiyo imekuja ni baada wa Mkuu wa Wilaya ya Geita,Mwl Herman Kapufi kutoa agizo la kujenga  visima hivyo mwaka jana mwezi wa kumi na mbili na kwamba kufikia tarehe thelathini mwezi wa tano mwaka huu wawe wamekamilisha ujenzi huo.

Akizungumza kwenye Mkutoni wa wananchi Diwani wa Kata ya Kaseme Andrea Kalamla amesema kuwa hadi sasa kuna kisima kimoja tu ambacho kimejengwa na chenyewe hakitoi maji hadi sasa hali ambayo imekuwa ikisababisha wanakijiji kutembea umbali mrefu kufuata maji.

“Mkuu wa Wilaya ungekuwa umefika mapema tungekupeleka kwenye kisima ambacho kimejengwa ambacho hakina ubora wowote kabisa kwani tunavyozungumza hadi sasa kisima kimekauka na hakina maji kabisa na mimi kila ninapofika hapa  wanakijiji wamekuwa wakiniomba maji hali ambayo imeendelea kuninyima amani”Alisema Kalamla.

Kwa upande wake meneja wa mgodi wa huo ,BW Simion Lubamba ameelezea kuwa utekelezaji wa ahadi za mgodi kwa wananchi zilikwama kutokana na uzalishaji kupungua hivyo amewaomba wananchi kumpa muda wa miezi miwili atakuwa ametekeleza ahadi hiyo.

“Kweli uhaba wa maji upo hapa kulingana na agizo lako ambalo uliliandika mwekezaji nilimpa nakala kwamba anatakiwa kutekeleza ahadi hiyo mwezi wa tano tarehe thelathini awe ametekeleza lakini alijibu kuwa hali ilikuwa ni mbaya hivyo ameomba kwa wananchi wampe miezi miwili hatakuwa atahakikisha anatekeleza ahadi hiyo”Alisema Lubamba.

Kutokana na maelezo hayo Mkuu wa Wilaya Mwl Herman Kapufi akatoa maagizo kwa afisa madini juu kufungia mgodi huo hadi pale utakapo tekeleza ahadi yake huku mkuu wa jeshi la polisi wilayani hapo akitakiwa kuweka   ulinzi wa kutosha .

Wanakijiji wa kijiji hicho wamepongeza kwa hatua ambayo ameichukua Mkuu wa Wilaya huku wakidai ni bora wote wakakoswa.

Akizungumzia Sheria ya madini kuhusu wawekezaji Afisa madini wa Mkoa wa Geita,Ally Said Ally amesema kuwa mwekezaji anapaswa kutoa huduma za kijamii .

IMEANDALIWA NA MADUKA ONLINE

.

Share it:

habari

Post A Comment: