WAZIRI MKUU "VIONGOZI WA MADHEHEBU YA DINI HAWANA BUDI KUENDELEA KUHUBIRI AMANI NA KULIOMBEA TAIFA"

Share it:
1
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akishiriki  katika swala ya magaharibi katika  futari iliyoandaliwa na Waziri Mkuu mjini  Chato, mkoani Geita, Juni 21, 2017. 
2
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akisalimiana na Askofu Mussa Magwesera wa Kanisa la African Inland Church (AIC), Dayosisi ya Geita katika futari iliyoandaliwa na Waziri Mkuu kwa Niaba ya Rais John Pombe Magufuli  mjini  Chato mkoani Geita  Juni 21, 2017.
3
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akifuturu pamoja na Askofu Mussa Magwesera wa Kanisa la African Inland Church (AIC)  Dayosisi ya Geita (kushoto) na Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Geita, Alhaj Yusuph Kabaju(kulia) katika futari iliyoandaliwa na Waziri Mkuu kwa niaba ya Rais John Pombe Magufuli, mjini  Chato, mkoani Geita  Juni 21, 2017.


Serikali  imewataka viongozi  wa madhehebu  ya dini nchini  kutumia  majumba  yao  ya ibada  kuhubiri  amani  badala  kuhubiri  mahubiri  yanayo weza  kusababisha  mifarakano  na jamii .
Kauli   hiyo  imetolewa   jana  na Waziri  Mkuu  wa    Kassimu  Majaliwa  wakati  akifuturu na    waumuni  wa dini  ya kislamu  mjini  Chato  mkoani Geita  futari ambayo  imeandaliwa na Rais  wa awamu  ya tano  Dk, John  Pombe  Magufuli.

Alisema  kuwa  viongozi  wa madhehebu  ya dini  hawana  budi  kuendelea kuhubiri  amani  na kuliombea Taifa  wakati  wote  ili kudumisha  amani  na upendo  ambao tumeachiwa  na wa  waasisi   wa Taifa hili akiwemo  Baba wa Taifa  mwalimu  Julius  Kambarage  Nyerere badala  ya kuibua  mifarakano ndani ya makanisa  kama kugombea  madaraka .

Waziri  mkuu  alisema   kuwa  serikali  ya awamu  ya  tano  inaheshimu  na kuthamini   mchango  wa  madhehebu  ya dini  katika kuliombea  Taifa  amani  na kwamba  kila mmoja  anayo haki ya kuabudu  katika imani yake ya dini na hivyo  kuwataka  viongozi hao  kudumisha tunu ya amani  ambayo  Mungu  amewajalia  watanzania  .

Majaliwa  ameongeza  kuwa  madhehebu  ya dini yana saidia watoto kuwalea katika maadili mema   na kuishi  katika njia zinazo mpendeza    Mungu huku akiwataka  kuwalea watoto  wao katika maadili ya kumjua Mungu  .
Aidha  waziri  huyo  aliwataka  waumini  wa dini ya kislamu tumia kipindi cha mwezi mtukufu  wa  ramadhani   kumuomba  mwenyezi    Mungu   kupendana  pamoja  na kuvumiliana 

“Serikali  ya  awamu  ya tano  ina thamini  mchango wa madhehebu  ya dini  kila mtu ana haki na uhuru wa kuabudu  na kuamini  katika imani yake  ya dini  hivyo  viongozi  wa madhehebu  tumieni  majumba yenu  ya  ibadaa    kuhubiri  amani na kuliombea  Taifa”alisema  majaliwa .

Mwenyekiti  wa umoja  wa  madhehebu  ya dini mbalimbili  Mkoani  humo ( INTER  FAITH )  Askofu  Mussa  Magwesela  akitoa salamu  za umoja  huo alimpongeza  Rais  Magufuli  pamoja  na makamu wa Rais Samia   Hassani  Suluhu  na waziri mkuu kwa utendaji  wao wa kazi kwa kipindi cha  miezi kumi na nane tangu  waingie madarakani .

Shekhe  mkuu wa mkoa wa Geita  Alihaji  Yusufu  Kabaju  aliwataka waumini  wa kislamu na jamii kwa jumla kumuomb  Mungu  na   kudumisha  amani  na upendo .
Awali  katibu  wa baraza  la bakwata  wilayani Chato Shekh  Ally    Motondi  akisoma  risala mbele ya waziri mkuu  alisema kuwa asiyeshukuru  mazuri  ata kwa Mungu  hawezi kushukuru  huku akimpongeza  Dk  Rais  Magufuli  kwa  kwa futari  hiyo .

IMEANDALIWA NA MADUKA ONLINE
Share it:

habari

Post A Comment: