Spika wa
Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (wa pili kulia)akifanya mazungumzo na Kiongozi wa
Chama cha Kikomunisti cha Urusi na kiongozi wa Bunge la nchi hiyo, Komredi
Gennady Zyuganov (wa pili kushoto) alipomtembelea leo ofisini kwake katika maadhimisho
ya miaka 100 ya Mapinduzi Makuu ya Urusi. Mheshimiwa Spika yupo nchini Urusi, akishiriki
Mkutano wa 137 wa Chama cha Mabunge Duniani unaoendelea leo Jijini St. Petersburg,
Urusi
Spika
wa Bunge Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto) akimkabidhi zawadi Kiongozi wa Chama
cha Kikomunisti cha Urusi na kiongozi wa Bunge la nchi hiyo Komredi Gennady
Zyuganov (katikati) alipomtembelea ofisini kwake. Kulia ni Balozi wa Tanzania
nchini huko, Jenerali Mstaafu Wynjones kisamba. Mheshimiwa Spika yupo nchini
humo kushiriki mkutano wa 137 wa Chama cha Mabunge Duniani.
Spika wa
Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto) akivishwa nishani maalum ya
maadhimisho ya miaka 100 ya Mapinduzi Makuu ya Urusi na Kiongozi wa Chama cha
kikomunisti cha Urusi, Komredi Gennady Zyuganov ambae ni Kiongozi wa Chama cha
Kikomunisti cha Urusi na kiongozi wa Bunge la nchi hiyo alipomtembelea ofisini
kwake. Mheshimiwa Spika yupo nchini humo akishiriki Mkutano wa 137 wa Chama cha
Mabunge Duniani.
Post A Comment: