RAIS MAGUFULI"TANZANIA NI NCHI YA TANO KWA UKUAJI WA UCHUMI BARANI AFRIKA"

Share it:
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Pombe Magufuli akihutubia mamia ya wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wa uzinduzi wa barabara ya Uyovu-Bwanga yenye urefu wa kilomita 45.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Pombe Magufuli  akiingia kwenye viwanja vya Kanisa la Romani Uyovu ambapo ndipo ufunguzi wa Barabara ya  Uyovu-Bwanga yenye urefu wa kilomita 45 ulipofanyikia.

Mamia ya wananchi Wilayani Bukombe Mkoa wa Geita wakifuatilia  Burudani ya Kwaya ambayo ilikuwa ikiimba (haipo kwenye picha) wakati wauzindua barabara ya Uyovu-Bwanga yenye urefu wa kilomita 45.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Pombe Magufuli akifurahia kutokana na nyimbo ambayo ilikuwa ikiimbwa na Kwaya ya Uyovu.

Mkuu wa mkoa wa Geita,Mhandisi Robert Luhumbi akiwatambulisha baadhi ya wageni ambao walikuweo kwenye shughuli ya uzinduzi wa Barabara ya Uyovu-Bwanga.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Pombe Magufuli na Mkuu wa mkoa wa Geita Mhandisi Robert Luhumbi wakimsikiliza Mbunge wa Jimbo la Bukombe Doto Biteko.

Mbunge wa Jimbo la Bukombe ambaye pia ni Naibu Waziri wa Madini Mhe Doto Mashaka Biteko akimshuku Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Pombe Magufuli kwa fedha zilizotolewa na serikali kwa ajili ya ujenzi wa shule na vituo vya afya Wilayani bukombe wakati wa dhifa ya uzinduzi wa barabara ya Uyovu-Bwanga yenye urefu wa kilomita 45.

Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhe.  Elias Kwandikwa akielezea namna shughuli za ujenzi wa barabara ya Uyovu-Bwanga zilivyofanyika.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Pombe Magufuli akikata utepe ishara ya uzindua wa barabara ya Uyovu-Bwanga yenye urefu wa kilomita 45.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na Mjumbe wa halmashauri kuu ya Taifa ya chama cha mapinduzi(CCM) Mkoani Geita Iddi Kassim Iddi.



Na,Joel Maduka,Geita.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Pombe Magufuli amesema Tanzania ni nchi ya tano kwa ukuaji wa uchumi barani Afrika hivyo wananchi wanapaswa kuwapuuza wanasiasa wanaohubiri kuporomoka kwa uchumi kwa matakwa ya kujiimarisha kisiasa.

Hayo ameyasema Leo kwenye shughuli ya uzinduzi rasmi wa barabara ya Uyovu-Bwanga yenye urefu wa kilomita 45 ambayo imekamilika kwa kujengwa kwa kiwango cha lami.

Katika dhifa hiyo iliyofanyika katika Kijiji cha Runzewe Kata ya Uyovu Wilaya ya Bukombe Mkoani Geita, Rais Magufuli Alisema katika kipindi cha miaka miwili serikali imefanya kazi kubwa ikiwa ni pamoja na kuimarisha sekta mbalimbali kwa usimamizi mzuri katika rasiliamali Madini, kuboresha sekta ya elimu ambapo wanafunzi wanasoma bure kuanzia ngazi ya msingi hadi sekondari.

Alisema kuwa, bajeti ya mwaka 2015 katika sekta ya afya ilikuwa ni Bilioni 31 lakini serikali kwa kutambua umuhimu wa kuimarisha afya za watanzania ambapo sasa bajeti imefikia shilingi Bilioni 239 na hayo ni matokeo ya umoja na amani iliyopo nchini.

Rais Magufuli ameendelea kusisitiza suala la  amani iliyopo nchini Tanzania kwamba imejengwa chini ya muasisi  Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, ikasimamiwa vyema na marais wastaafu Mhe Ally Hassan Mwinyi, Mhe Benjamin Mkapa pamoja na Mhe Jakaya Mrisho Kikwete.

"Mambo yanayofanywa na serikali hayawezi kuyafurahisha mataifa mengine hivyo mataifa hayo yanawatumia watanzania wenyewe kutengeneza chuki dhidi ya serikali yao" Alisema  Rais Magufuli.

Aliongeza kuwa kukamilika kwa barabara hiyo imekuwa sehemu ya Kuchochea shughuli za maendeleo ya kijamii katika usafirishaji wa mazao, kurahisisha usafirishaji wa watu na bidhaa, sambamba na kuongeza pato la Mkoa wa Geita na Taifa kwa ujumla.

Katika hatua nyingine Rais Magufulu amewasihi wananchi Kutovamia hifadhi za Taifa badala yake kuwa wavumilivu na kuiacha serikali ifanye, kwani watatumwa wataalamu wa Wizara ya ardhi na maliasili ili kuratibu na kuona namna ya kuyagawa maeneo kwa ajili ya wafugaji na wakulima.

Naye, Naibu Waziri wa Ujenzi Mhe Elius John Kuandikwa na Mtendaji Mkuu wa Tanroads nchini Mhandisi Patrick Mfugale walisema kuwa usanifu wa barabara hiyo ulifanywa mwaka 2006 na kampuni mbili za kitanzania kwa jumla ya Shilingi Milioni 207.6 ambapo barabara hiyo imesanifiwa kubeba na kutumika kwa miaka 20 kwa upana wa mita 9.5

Walisema Ujenzi wa barabara hiyo uliokamilika Octoba mwaka jana umegharimu jumla ya shilingi Bilioni 45.454, ambapo msimamizi amelipwa shilingi Bilioni 2.3 huku akiendelea kuwa chini ya uangalizi wa mkandarasi hadi mwezi Octoba mwaka huu. 

Dhifa ya uzinduzi wa barabara hiyo umehudhuriwa na Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel, Naibu Waziri wa Ujenzi, uchukuzi na mawasiliano, Mhe Elius John Kuandikwa, Mbunge wa Jimbo la Bukombe ambaye pia ni Naibu waziri wa Madini Mhe Doto Mashaka Biteko, Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Joseph Nyamhanga na Mtendaji Mkuu wa Tanroads Mhandisi Patrick Mfugale.

Share it:

habari

Post A Comment: