Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Pombe Magufuli akihutubia mamia ya wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wa uzinduzi wa barabara ya Uyovu-Bwanga yenye urefu wa kilomita 45. |
Mamia ya wananchi Wilayani Bukombe Mkoa wa Geita wakifuatilia Burudani ya Kwaya ambayo ilikuwa ikiimba (haipo kwenye picha) wakati wauzindua barabara ya Uyovu-Bwanga yenye urefu wa kilomita 45. |
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Pombe Magufuli akifurahia kutokana na nyimbo ambayo ilikuwa ikiimbwa na Kwaya ya Uyovu. |
Mkuu wa mkoa wa Geita,Mhandisi Robert Luhumbi akiwatambulisha baadhi ya wageni ambao walikuweo kwenye shughuli ya uzinduzi wa Barabara ya Uyovu-Bwanga. |
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Pombe Magufuli na Mkuu wa mkoa wa Geita Mhandisi Robert Luhumbi wakimsikiliza Mbunge wa Jimbo la Bukombe Doto Biteko. |
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhe. Elias Kwandikwa akielezea namna shughuli za ujenzi wa barabara ya Uyovu-Bwanga zilivyofanyika. |
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Pombe Magufuli akikata utepe ishara ya uzindua wa barabara ya Uyovu-Bwanga yenye urefu wa kilomita 45. |
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Pombe
Magufuli amesema Tanzania ni nchi ya tano kwa ukuaji wa uchumi barani Afrika
hivyo wananchi wanapaswa kuwapuuza wanasiasa wanaohubiri kuporomoka kwa uchumi
kwa matakwa ya kujiimarisha kisiasa.
Hayo ameyasema Leo kwenye shughuli ya uzinduzi rasmi wa barabara
ya Uyovu-Bwanga yenye urefu wa kilomita 45 ambayo imekamilika kwa kujengwa kwa
kiwango cha lami.
Katika dhifa hiyo iliyofanyika katika Kijiji cha Runzewe Kata ya
Uyovu Wilaya ya Bukombe Mkoani Geita, Rais Magufuli Alisema katika kipindi cha
miaka miwili serikali imefanya kazi kubwa ikiwa ni pamoja na kuimarisha sekta
mbalimbali kwa usimamizi mzuri katika rasiliamali Madini, kuboresha sekta ya
elimu ambapo wanafunzi wanasoma bure kuanzia ngazi ya msingi hadi sekondari.
Alisema kuwa, bajeti ya mwaka 2015 katika sekta ya afya ilikuwa
ni Bilioni 31 lakini serikali kwa kutambua umuhimu wa kuimarisha afya za
watanzania ambapo sasa bajeti imefikia shilingi Bilioni 239 na hayo ni matokeo
ya umoja na amani iliyopo nchini.
Rais Magufuli ameendelea kusisitiza suala la amani iliyopo nchini Tanzania kwamba imejengwa
chini ya muasisi Hayati Mwalimu Julius
Kambarage Nyerere, ikasimamiwa vyema na marais wastaafu Mhe Ally Hassan Mwinyi,
Mhe Benjamin Mkapa pamoja na Mhe Jakaya Mrisho Kikwete.
"Mambo yanayofanywa na serikali hayawezi kuyafurahisha
mataifa mengine hivyo mataifa hayo yanawatumia watanzania wenyewe kutengeneza
chuki dhidi ya serikali yao" Alisema Rais Magufuli.
Aliongeza kuwa kukamilika kwa barabara hiyo imekuwa sehemu ya
Kuchochea shughuli za maendeleo ya kijamii katika usafirishaji wa
mazao, kurahisisha usafirishaji wa watu na bidhaa, sambamba
na kuongeza pato la Mkoa wa Geita na Taifa kwa ujumla.
Katika hatua nyingine Rais Magufulu amewasihi wananchi Kutovamia
hifadhi za Taifa badala yake kuwa wavumilivu na kuiacha serikali ifanye, kwani
watatumwa wataalamu wa Wizara ya ardhi na maliasili ili kuratibu na kuona namna
ya kuyagawa maeneo kwa ajili ya wafugaji na wakulima.
Naye, Naibu Waziri wa Ujenzi Mhe Elius John Kuandikwa
na Mtendaji Mkuu wa Tanroads nchini Mhandisi Patrick Mfugale walisema
kuwa usanifu wa barabara hiyo ulifanywa mwaka 2006 na kampuni mbili za
kitanzania kwa jumla ya Shilingi Milioni 207.6 ambapo barabara hiyo imesanifiwa
kubeba na kutumika kwa miaka 20 kwa upana wa mita 9.5
Walisema Ujenzi wa barabara hiyo uliokamilika Octoba mwaka jana
umegharimu jumla ya shilingi Bilioni 45.454, ambapo msimamizi amelipwa shilingi
Bilioni 2.3 huku akiendelea kuwa chini ya uangalizi wa mkandarasi hadi mwezi
Octoba mwaka huu.
Dhifa ya uzinduzi wa barabara hiyo umehudhuriwa na Mkuu wa Mkoa
wa Geita Mhandisi Robert Gabriel, Naibu Waziri wa Ujenzi, uchukuzi na
mawasiliano, Mhe Elius John Kuandikwa, Mbunge wa Jimbo la
Bukombe ambaye pia ni Naibu waziri wa Madini Mhe Doto Mashaka Biteko, Katibu
Mkuu wa Wizara ya Ujenzi uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Joseph
Nyamhanga na Mtendaji Mkuu wa Tanroads Mhandisi Patrick Mfugale.
Post A Comment: