BAJAJI WAGOMA KUTOA HUDUMA YA USAFIRI GEITA

Share it:
Bajaj zikiwa zimepakiwa na waendeshaji mjini Geita baada ya kuwa na madai ya kuonewa na askari.

Bw,Joseph Dotto ambaye ni mwendesha bajaji mjini Geita akilalamika juu ya kamata kamata ambayo inaendelea mjini humo.



Waendesha Bajaji Mjini Geita Mkoani Humo wamelilalamikia jeshi la Polisi kuendelea kuwakamata pasipokujua makosa yao ni nini na kujikuta wakishindwa kuendelea kufanya kazi zao kwa amani hali ambayo imepelekea kutokuendelea na kazi zao za usafirishaji wa abiria.

Wamesema hali hiyo imeendelea kuwaathiri kutokana na wengi wao kukopa bajaji hizo na kutegemea kufanya kazi hili waweze kurudisha madeni ambayo wanadaiwa na kampuni za usafiri huo.

Bajaj ndio usafiri maarufu  mjini  Geita kwa mizunguko ya hapa na pale lakini Waendesha Bajaji wamejikuta wakisitisha kuendelea kufanya kazi zao kutokana na kuwa na malalamiko ya kukamatwa  na kutozwa faini kubwa bila ya kujua makosa yao.

“tumeendelea kukamatwa na kupigwa faini pasipokujua makosa yetu ni nini hata tukiuliza hatujibiwi tunakamatwa na kuambiwa twende kituoni tena na askari ambao wanakuwa wamevaa nguo za kirahia je hiyo ni haki kweli sasa hivi ninasiku mbili sifanyi kazi watoto wangu wamelala na njaa sijajua tatizo ni nini hadi kufikia hatua ya kukamata bajaji zetu”Alisema Bw,Mussa Kisoke.

Hata hivyo baadhi yao wameelezea kuwa pamoja na kukamilisha usajili wa bajaji zao na kuwa na kila kitu bado wameendelea kukutana na dhoruba la kamata kamata inayoendelea kwa sasa mjini humo.
“Sisi hizi bajaji tumezikopa na tunarejesha marejesho kwa wiki na isitoshe zingine zimekamilisha kila kitu kwa maana ya bima,Sumatra na leseni lakini tunakamatwa na kupigwa faini kiuweli tunaumia sana”Alisema Joseph Dotto.

Kutokana na malalamiko hayo kuliangukia Jeshi la Polisi  kamanda wa Polisi Mkoani Geita,Mponjoli Mwabulambo amesema msoko unaendelea kutokana na mambo ya ukiukaji masuala ya usalama barabarani na kwamba wataendelea kuwakamata wale wote ambao wameendelea kukiuka kanuni na taratibu za usalama Barabarani.

“Sababu ni uwegeshaji hivyo barabarani kwa maana wanasimama sehemu ambazo sio sahihi ninachotaka kusema kwamba hatuwaonei na tumeshakaa tukaongea nao maana tumeshatoa elimu na utaki kutuelewa tutachukua hatua”Alisema Kamanda Mponjoli.

Share it:

habari

Post A Comment: