BRAZIL YAINYUKA ARGENTINA 3-0 KUFUZU KOMBE LA DUNIA

Share it:

Timu ya Brazil imeitwanga Argentina ya Lionel Messi jumla ya magoli 3-0 katika michuano ya kuwania kufuzu kombe la Dunia itakayochezwa nchini Urusi mwaka 2018.

Brazil walianza kuliona lango la akina Messi dakika ya 24 Philipo Countinho aliwanyanyua washabiki kwa goli safi akipokea pasi toka Neymar kabla timu hazijaenda mapumziko Neymar alifunga goli la pili mnomo dakika ya 45 hadi mapumziko wenyeji walikuwa mbele.

Kipindi cha pili kilianza kwa Argentina kujaribu kutafuta angalau hata goli walishindwa kupita ukuta wa wenyeji katika dakika ya 59 kiungo wa zamani wa Tottenham Spurs kwa sasa anacheza soka nchini China Paulinho alifunga goli la tatu na kupeleka kilio kwa mashabiki wa Argentina hadi mwamuzi wa mchezo huo anapuliza kipenga cha mwisho Brazil wameibuka na ushindi wa magoli 3-0.

Kwa matokeo hayo Brazil wameendelea kubaki kileleni wakiwa na pointi 24 wakati Argentina wameshuka hadi nafasi ya sita wakiwa na pointi 16 ya msimamo wa hatua ya kufuzu kombe la Dunia 2018.

VIKOSI:Brazil: Alisson; Alves, Miranda (Silva 87), Marquinhos, Marcelo; Fernandinho, Paulinho, Renato Augusto; Coutinho (Costa 84), Neymar, Gabriel Jesus (Firminho 82)

Goals: Countinho 24, Neymar 45, Paulinho 59

Yellow cards: Fernandinho, Marcelo

Argentina: Romero; Zabaleta, Otamendi, Funes Mori, Mas; Perez (Aguero 46), Biglia, Mascherano, Di Maria (Correa 71); Messi, Higuain

Yellow cards: Biglia, Otamendi, Funes Mori.

Matokeo mengine ya kufuzu kombe la Dunia ni:

Uruguay 2-1 Ecuadur.

Venezuel 5-0 Bolivia.

Paraguay 1-4 Peru.


Share it:

michezo

Post A Comment: