BAADHI YA MAENEO YA VIJIJI VYA CHATO YAKUBWA NA UKAME.

Share it:
Shamba la Mahindi ambalo limekauka kutokana na hali ya ukame kwenye kijiji cha Nyan’homango Kata ya Ilemela kilichopo Wilayani Chato. 

Mbunge wa Jimbo la Chato ambaye pia ni Waziri wa Nishati,Dk Medard Kalemani akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Nyan’homango Kata ya Ilemela wakati alipofika kuangalia utekelezaji wa mradi wa REA awamu ya Tatu kijijini Hapo. 

Mwenyekiti wa Kijiji cha Nyan’homango Bw,Lameck Kajile akielezea changamoto ambazo zimejitokeza kutokana na hali ya ukame kijiji hapo. 

Fundi mitambo akiweka vyombo vya musiki sawa wakati wa ziara ya Waziri wa Nishati Kwenye Kijiji cha Nyan’homango. 

Wnanchi wa kijiji cha Nyan’homango Kata ya Ilemela  wakiwa kwenye mkutano wa mbunge wa jimbo la chato.
Mkuu wa Wilaya ya Chato,Shaaban Ntarambe akiwashukuru wananchi ambao walijitokeza kwenye mkutano wa mbunge wa Chato.



Na,Joel Maduka,Chato
Wakati neema ya mvua ikiendelea Mkoani Geita,Baadhi ya maeneo Wilayani Chato yamekubwa na ukame ambao umesababisha mazao ya wakulima kukaukia mashambani.

Baadhi ya maeneo hayo ni  pamoja na kijiji cha Nyan’homango Kata ya Ilemela ambapo mahindi yamekaukia mashambani kutokana na hali ya kukosekana kwa mvua kwa muda mrefu kwenye maeneo hayo .

Mkuu wa wilaya Shambani Ntarambe akizungumza na kutoa taarifa ya Wilaya Hiyo mbele ya Mbunge wa Jimbo la Chato Dkt,Medard Kalemani ,amesema kuwa maeneo mengi yameathirika kutokana na ukame hata hivyo amewataka wakulima kulima mazao mbadala na yanayositahimili  ukame ikiwemo zao la Mtama ili kuepukana na baa la njaa hapo baadae iwapo hali  hiyo itaendelea.

Wakizungumza baadhi ya wananchi na wakulima wa Kijiji cha Nyan’homango akiwemo afisa mtendaji wa kijiji hicho Malimi Mkano wameelezea kuwa hali hiyo imewaathiri kwa kiasi kikubwa kutokana na kwamba wengi wao walikuwa wanategemea mahindi ambayo yamekaukia shambani kupata chakula na kwamba awakujua kama hali ya hewa itaweza kubadilika.


Kwa upande wake Mbunge wa Chato Dk. Kalemani ameelezea kuwa mazao hayajaharibika sana na kwamba mazao mengi bado yapo vizuri pamoja na changamoto za hali ya hewa bado wanamatarajio ya kupata chakula kingi kwenye Wilaya hiyo na kwamba ameendelea kusisitiza wakulima kulima mazao ambayo yanasitahimili hali ya ukame.
Share it:

JOEL MADUKA

habari

Post A Comment:

Also Read

WATORO 1,957 WAPEWA SIKU SABA KURUDI SHULENI

Mkuu wa Mkoa Geita Mhandisi Robert Gabriel ametoa siku saba kwa wazazi wa wanafunzi 1,957 wa shule za

JOEL MADUKA