KICHANGA CHA SIKU MOJA CHAFUKULIWA BAADA YA KUZIKWA.

Share it:



Mzee Didas Shitobero,Akionesha eneo ambalo limechimbuliwa na kutolewa kichanga hicho.

Mzee Didas Shitobero,akielezea namna tukio lilivyokuwa.

Akiwa na jirani yake wa karibu .

Haya ni makazi ya kwa Mzee Didas Shitobero.

Mwenyekiti wa kitongoji ,Mathias Bumbuli akielezea namna alivyoguswa na tukio hilo





GEITA :Katika hali isiyo ya kawaida familia ya mzee Didasi Shitobero, wa kijiji na kata  Bugulula ,Wilayani na Mkoani Geita,wamejikuta wakiingiwa na hofu kubwa  kutokana na kukutwa kitoto kichanga  cha siku moja kilichozaliwa kikiwa kimefariki  kimefukuliwa nyuma ya nyumba yake.

Maduka online imefika kijiji hapo na kujionea kaburi la mtoto huyo wa siku moja likiwa limefukuliwa na mwili kutolewa ndani ya kaburi hilo.
Baba wa familia hiyo, Didasi Shitobero alisema  kuwa tukio hilo lilitokea jumatatu ambapo baada ya kuamka siku hiyo walikuta kaburi la mtoto likiwa limefukuliwa na mwili hakuwemo katika kaburi hilo.

“Tumesikitishwa sana na kitendo hiki cha kufukuliwa kwa mtoto mchanga kwani tumeshindwa kujua ni nani ambae amefanya kitendo cha namna hii ambacho ni cha kinyama kabisa”alisema Shitobero.

Kutokana na tukio hili kuwasitajabisha baadhi ya majirani kwa kufukuriwa kwa kichanga hicho walisema  kuwa wale wote ambao wamekuwa na tabia za namna hiyo ni vyema wakaachana nazo kwani imani hizo sio nzuri.

Kutokana na ukubwa wa swala hili  madukaonline ilibidi imtafute mwenyekiti wa zengo Mathias Bumbuli,alisema ni vyema kwa jamii iliyopo katika eneo ambalo analiongoza wakaachana na maswala ya imani za kishirikina kwani hakuna faida yoyote ambayo mtu anaweza kupata kwa kufanya maswala hayo.

Imeandaliwa na Joel Maduka
Share it:

matukio

Post A Comment: