MAJAMBAZI YAKAMATWA NA SILAHA ZA VITA NA SARE ZA POLISI

Share it:

JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limefakiwa kukamata watu watatu wanaodaiwa kuwa ni majambazi hatari ambao wamekuwa wakishiriki matukio mbalimbali ya uhalifu kwa kutumia silaha. 



Watu hao wanaodaiwa kuwa majambazi walipatikana na bunduki 23 za aina tofauti tofauti, Risasi 835, kifaa cha kuzuia risasi kuingia mwilini tatu (Burret Proof), Sare za Polisi, Pingu 48 pamoja na Radio 12 za mawasiliano. 



Akizungumza na waandishi wa habari katika viwanja vya kanda maalum, Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam Kamishna, Simon Sirro amesema kuwa majambazi hao walikuwa na mtandao mkubwa ikiwa ni kununua silaha nje ya nchi kwa ajili ya kufanyia uhalifu katika maeneo mbalimbali. 



Kamanda Sirro amesema baada ya tukio hilo timu ya polisi ya upelelezi iliweka mtego na kufanikiwa kukamata majambazi watatu maeneo ya Mbagala, Keko na Kawe. 



Kamanda Sirro amesema katika mahojiano walikiri kufanya tukio katika benki ya Habib African maeneo ya Kariakoo 2014 na Stanbic 2014. 


Amesema kuwa majambazi walikiri kuwa na wenzao wako katika msitu wa Vikindu. Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii. 
Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum Dar es Salaam, Kamishina Simon Sirro akionyesha kifaa cha kuangalia wakati wakifanya uhalifu majambazi kwa waandishishi wa habari ikiwa ni sehemu ya vifaa vilivyokuwa vikitumika na majambazi sugu leo katika viwanja vya ofisi ya kanda maalum leo jijini Dar es Salaam. 

Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum Dar es Salaam, Kamishina Simon Sirro akionyesha bunduki kwa waandishi wa habari ikiwa ni sehemu yabunduki zilivyokuwa zikitumika na majambazi sugu leo katika viwanja vya ofisi ya kanda maalum leo jijini Dar es Salaam. 
Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum Dar es Salaam, Kamishina Simon Sirro akizungumza na waandishi habari juu ya operesheni walioifanya na kukamata majambazi watatu katika viwanja vya ofisi ya kanda maalum leo jijini Dar es Salaam

.














Share it:

habari

matukio

Post A Comment: