WAVUVI KATA YA NKOME WALALAMIKIA KUONEWA NA WATU KUTOKA IDARA YA UVUVI

Share it:
Wavuvi wa mwalo wa Makatani kata ya Nkome  wilayani Geita wakiendelea na maandalizi kwaajili ya kwenda kwenye shughuli ya uvuaji wa dagaa.

Dhana za uvuvi ambazo wamelalamikiwa kuwa zinakamatwa na maafisa uvuvi kwa madai kuwa zinashiri kwenye suala la uvuvi haramu.

Mzee Yohana Kulwa akielezea masikitiko yake kutokana na suala kuendelea kukamatwa na kupigwa faini na watu wa idara ya uvuvi bila ya kuwa na makosa yoyote.



Wavuvi wa Mwalo wa makatani Kata ya nkome Wilaya na Mkoa wa Geita,wamelalamikia kuonewa na watu kutoka idara ya uvuvi kutokana na kuendelea kuwakamata na kuwapiga faini pasipokuwa na makosa yoyote yale hali ambayo imeendelea kuwatia hofu pindi wanapokuwa wanatekeleza majukumu yao.

Hatua hiyo imekuja ni kutokana na msako ambao unaendelea ziwa Viktoria wa kuwakamata watu ambao wameendelea kujihusisha na shughuli za uvuvi haramu.

Wakizungumza na mtandao huu ,baadhi ya wavuvi hao wamesema kuwa pamoja na kuendelea kutii sheria kwa kutumia zana za uvuvi ambazo zinakubalika kwa mujibu wa sheria bado wameendelea kukamatwa na kupigwa faini na watu wa idara ya uvuvi.

Mwenyekiti wa kitongoji hicho ,Bi  Anna Peter na Mwenyekiti wa BMU Bw,Peter John wamedai kutokushirikishwa kwenye shughuli hiyo ya kukamata watu hao na kwamba  elimu bado  ni tatizo kwa wavuvi wengi kutokujua ni zana zipi ambazo zinatumika kwenye shughuli zao kutokana na kutokupewa elimu.

Hata hivyo kwa upande wake diwani wa kata hiyo,Masumbuko Nsembe amesema malalamiko ya wavuvi hao amekwisha kuyapeleka halmashauri na kwamba hadi sasa yanafanyiwa kazi.

Mtandao huu  umemtafuta Mkuu wa oparesheni hiyo,Bw Roman Mkenda kwa njia ya simu ambapo amesema   kuwa baadhi ya wavuvi wamekuwa wakikimbia pindi wanapowaona hali ambayo inasababisha  wao kujua kuwa ni  mvuvi haramu na kwamba suala la elimu wamekuwa wakilitoa pindi mtu anapoomba kibali cha kutaka kuwa mvuvi.



Share it:

habari

Post A Comment: